Na Mwandishi Wetu
Kuelekea mchezo wa mkondo wa pili kuwania kufuzu hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Barani Afrika CAF CC, Uongozi wa klabu ya Club Africain umetoa tafadhali kwa mashabiki wake.
"Bodi ya Wakurugenzi ya Club Africain inawataka mashabiki wake kuwa waangalifu, kujizuia na kutojihusisha kabisa na fujo (kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Yanga)" imeeleza taarifa hiyo.
Kupitia mtandao wa kijamii muda huu klabu hiyo imetoa tamko hilo ikiwataka wasifanye kitendo chochote cha uvunjifu wa taratibu kama waliofanyiwa wao Dar es Salaam.
Bodi hiyo imesisitiza umuhimu wa nidhamu katika kuheshimu sheria za mashindano ili kuepusha timu yao kupata adhabu kutoka (CAF).
Ikumbukwe tayari klabu hiyo imeonywa na iko chini ya uangalizi wa (CAF).
November 09, 2022
Home
Unlabelled
CLUB AFRICAIN YAWAONYA MASHABIKI WAKE
CLUB AFRICAIN YAWAONYA MASHABIKI WAKE
Share This
About HABARI MSETO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Ut wisi enim ad minim veniam, quis nostrud exerci tation ullamcorper suscipit lobortis nisl ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis autem vel eum iriure dolor in hendrerit in vulputate velit esse molestie consequat.





No comments:
Post a Comment