Na Mwandishi Wetu
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo. Saidi Yakubu amesema Tanzania inakwenda kunufaika kiuchumi na kiutamaduni kwenye msimu ya utamaduni wa Afrika ya kusini unaoanza leo kwa muda wa wiki moja nchini Tanzania.
Amezitaja baadhi ya faida ambazo Tanzania itanufaika nazo kuwa kupitia onesho la saana za ufundi mbalimbali, wasanii watapata ajira za muda.
Pia, kupitia maonesho ya kazi za sanaa, utamaduni na ubunifu, wasanii watapata fursa ya kuonesha na kuuza kazi zao za mikono;
Aidha, ameongeza kwamba kupitia msimu huu nchi hizo zinakwenda kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mkataba wa ushirikiano katika Sekta ya Utamaduni uliosainiwa mwaka 2011.
Faida nyingine ni Wasanii kubadilishana uwezo katika kufanya biashara ya kazi za sanaa na ubunifu kupitia Semina kwa wasanii itakayofanyika Novemba 23, 2022; na kuimarisha mbinu na njia ya uhifadhi na uendelezaji wa historia ya ukombozi wa Nchi za Kusini mwa Afrika.
Amesema msimu huu unakwenda kufunguliwa rasmi jioni ya leo na Waziri wa utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa.
No comments:
Post a Comment