HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 07, 2023

APRM ; SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAJITAHIDI KUTATUA KERO ZA WANANCHI

 

Na Magrethy Katengu


Katibu Mtendaji APRM Tanzania  Mpango wa hiari wa nchi za umoja wa Afrika kujipima kwa vigezo vya Utawala bora Lamau Mpolo amesema  Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan serikali imejitahidi kutatua kero za wananchi ikiwemo kusambaza huduma za maji, umeme, miundombinu, hospitali, shule 


Ameyasema hayo Jijini Dar es salaam wakati alipotembelea maonyesho ya sabasaba katika banda la APRM  ambapo amesema Tanzania kama mwanachama imekuwa ikipimwa kwa vigezo vilivyowekwa na tafiti hukusanywa kupitia maoni ya wananchi wanayotoa wenyewe na kubaini kuwa Tanzania inapiga hatua katika kutatua kero za wananchi.


" APRM Makao yake makuu yapo Afrika kusini na kila mwananchi mwanachama ambaye ameridhia kujiunga ana ofisi hivyo Tanzania iliridhia kujiunga mwaka 2004 na 2006 walianza shughulia zao za utafiti na Ofisi yake iko chini ya Wizara ya Mambo ya nje na Afrika Mashariki  ikiratibu masula ikiwemo siasa,maendeleo ya kiuchumi na usimamizi wake,utawala bora " amesema Lamau


Sambamba na hayo amesema wamekuwa wakibadilishana uzoefu nchi na nchi kwa kutathimini utendaji wa nchi na nchi kujifunza  mazuri ikiwemo masuala siasa, Utawala bora,maendeleo ya  uchumi na usimamizi wake na wamepanga kufanya tathimini ya nchi zote na kutoa ripoti mbele ya wakuu wa nchi


Amesema Serikali ya awamu ya sita katika tafiti zao walizofanya wameona kuna mabadiliko makubwa katika sekta binafsi kuwabadilishia baadhi ya sera na kusaidia  kuvutia wawekezaji kuja Tanzania 


Sanjari na hayo amesema  Tanzania kulikuwa  kero za Muungano zaidi ya 20 lakini APRM imesadia zimetatuliwa na kubakia kero 3 kwa kutoa tafiti zao pamoja na maoni kutoka kwa wananchi. 


Aidha APRM imekuwa ikishirikiana wadau mbalimbali ikiwemo REPOA,Chuo kikuu cha Dar es salaam watafiti wengine  kufanya tafiti na kutoa ripoti zao na ametoa wito kwa wananchi kutembelea banda hilo kuuliza maswali na kutoa maoni yao serikali iwafanyie.

No comments:

Post a Comment

Pages