HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 15, 2024

Dkt. Nchimbi atua Mwanza, kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020 - 2024

 


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na wananchi wa Jimbo la Misungwi, leo Agosti 14, 2024, mara baada ya kuwasili na kupokelewa Mkoa wa Mwanza, kuanza ziara ya siku 2 ya kikazi mkoani humo, akitokea Mkoa wa Geita.

Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu Balozi Nchimbi ameambatana na Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Issa Haji Usi Gavu, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa - Oganaizesheni, Ndugu Amos Gabriel Makalla, Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo na Ndugu Rabia Hamid Abdalla, Katibu wa NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa.

Malengo ya ziara hiyo ya Katibu Mkuu wa CCM ni pamoja na kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020 - 2024, kukagua na kuhamasisha uhai wa CCM, pamoja na kuzungumza na kuwasikiliza wananchi.

No comments:

Post a Comment

Pages