HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 07, 2013

CRDB YAFUNGUA TAWI JIPYA COCO PLAZA OYSTERBAY

 Jengo la Coco Plaza ambalo kuna Ofisi za CRDB.
Wateja wakipata huduma.
Kaimu Meneja wa benki ya CRDB tawi la Oysterbay, Godlisten  Mtei 

Kaimu Meneja wa benki ya CRDB tawi la Oysterbay, Godlisten  Mtei (kushoto) akitoa maelekezo ya huduma mbalimbali wanazotoa katika tawi hilo jipya kwa Waziri wa zamani wa Elimu, Joseph Mungai. Tawi hilo limefunguliwa hivi karibuni katika jengo la Coco Plaza jijini Dar es Salaam. Katikati ni Ofisa Masoko wa benki hiyo, Nasib Kalamba.  

Ofisa Masoko wa benki ya CRD, Nasib Kalamba (katikati) akitoa ufafanuzi kwa mteja wa benki hiyo, waziri wa zamani wa Elimu, Joseph Mungai kaatika tawi jipya la benki hiyo lililopo katika jengo la Coco Plaza jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Meneja wa Tawi hilo, Godlisten Mtei.
Ofisa wa benki ya CRDB, JacqlineSawe akitoa maelekezo kwa mteja wa benki hiyo katika tawi la Oysterbay lililopo katika jengo la Coco Plaza jijini Dar es Salaam. 
Ofisa Masoko wa benki ya CRD, Nasib Kalamba (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa mteja wa benki hiyo, waziri wa zamani wa Elimu, Joseph Mungai katika tawi jipya la Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Wateja wakipata huduma.
Maofisa wa benki ya CRDB wakiandisha wateha wapya katika eneo la Namanga jijini Dar es Salaam.
Kaimu Meneja wa benki ya CRDB tawi la Oysterbay, Godlisten  Mtei (kushoto) akitoa maelekezo 
ya huduma mbalimbali wanazotoa katika tawi hilo jipya kwa Waziri wa zamani wa Elimu, Joseph Mungai.
Ofisa wa benki ya CRDB, George Abraham kisaini baadhi ya nyaraka za kibenki.

DAR ES SALAAM, Tanzania

BENKI ya CRDB, imefungua tawi jipya  Osysterbay  jijini Dar es Salaam ikiwa na lengo la kuwafikia wateja wake, ambapo takribani  wateja 400 wamekuwa wakihudumiwa kila siku katika tawi hilo.

Tawi hilo limeanza kufanya kazi hivi karibuni, ambapo limeonekana kuwa ni msaada mkubwa kwa wakazi wa Osysterbay na maeneo ya jirani.

 Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana Kaim Meneja wa CRDB, Godlisten Mtei alisema lengo kubwa la kupeleka tawi hilo ni kuwapa huduma kwa ukaribu wateja wao waliopo katika eneo hilo.

 Alifafanua kwamba, tangu kuanzishwa kwake tawi limekuwa ni mkombozi kwa wateja mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara wakubwa na wadogo pamoja na watu mbalimbali.

 “Tawi letu linatoa huduma zote za kibenki, na tunazidi kuwakaribisha wateja wetu ili wajionee huduma bora zitolewazo na benko yetu na pia tunatoa huduma mbalimbali zikiwemo za; Mashine ya kutoa na kuweka fedha (ATM) ambayo hufanyakazi masaa 24”alisema.

Mtei alitaja huduma zingine kuwa ni pamoja na TemboCardVisa, Akaunti ya Hundi na ya watoto inayojulikana kama Junior Account pamoja, Malikia akaunti  ambayo ni maalum kwa wanawake na Akaunti ya Akiba.
 Hata hivyo aliongeza kuwa, tawi hilo litakuwa likitoa Akaunti ya Tanzanite, huduma za mikopo mbalimbali na huduma za bima ili kuzidi kuwapatia huduma bora wateja wao.

 Alisema kuwa tangu kuanzishwa kwake tawi limekuwa likitoa huduma ya kibenki kwa kutumia Simu ya mkononi (SimBanking), pamoja na Akaunti ya Wanafunzi ambayo inafahamika kama Scholar Account.

Meneja huyo aliwataka Wananchi na wateja wapya kutumia tawi hilo pekee katika eneo hilo ili kupata huduma za kibenki badala ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma hizo kwenye matawi yaliyombali.
Katika hatua nyingine Meneja Mauzo wa benki hiyo Richard Joseph alisema, katika harakati za kufanikisha wananchi wanajiunga na benki hiyo wameamua kuweka tawi katika eneo la Namanga jijini Dar es Salaam ambapo kwa siku zaidi ya watu 70 wanaojiunga na benki hiyo.

No comments:

Post a Comment

Pages