HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 15, 2013

OSCAR PISTORIUS AFIKISHWA MAHAKAMANI LEO

 Pistorius akiinamia chini kuhofia wapiga picha wakati akiwasili mahakamani alikoshitakiwa kwa tuhuma za kumpiga risasi na kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.

 Dada yake na Oscar Pistorius, Aimee (kushoto) akiondoka katika Hospitali ya Mamelod, huko Pretoria, ambako kaka yake alikuwa akipimwa akili kutokana na maujai ya mpenzi wake.
 Msemaji wa Jeshi la Polisi, Denise Beukes akithibitisha mbele ya vyombo vya habari juu ya kufikishwa mahakamani kwa mkimbiaji mahiri wa mbio za walemavu, Pistorius anayekabiliwa na shitaka la kumpiga na kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp.
 Baadhi ya nguo za wafungwa katika Gereza la Pretoria Central zikiwa zimeanikwa kwenye kamba nje ya gereza hilo ambalo Oscar Pistorius amesekwa rumande kutokana na tuhuma za kumuuza mpenzi wake Reeva Steenkamp.
Harakati mbalimbali zimekuwa zikifanywa na wananchi na makampuni mbalimbali nchini Afrika Kusini kuonesha kumuunga mkono shujaa wa nchi hiyo anayekabiliwa na shitaka la kuua, Oscar Pistorius. Pichani moja ya mabango yanayoonesha picha ya mkali huyo.
 Oscar Pistorius akicheza na mbwa wake pembeni ya bwawa la kuogelea lililo ndani ya nyumba yake.
Oscar Pistorius akicheza na Chui wake anayemfuga katika jumba lake la kifahari.

No comments:

Post a Comment

Pages