*LINA UWEZO WA KUHUDUMIA HOSPITALI
524
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefungua duka la Bohari Kuu
ya Dawa (MSD) katika Hospitali ya wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi ambalo litakuwa
na uwezo wa kuhudumia hospitali 524 katika mikoa ya Lindi, Mtwara na wilaya ya
Tunduru mkoani Ruvuma.
Akizindua duka hilo leo (Jumamosi, Julai 16, 2016) Waziri
Mkuu amesema duka hilo litaendelea kuboresha huduma za upatikanaji wa dawa kwa
gharama nafuu katika hospitali, vituo
vya afya na zahanati katika wilaya ya Ruangwa pamoja na mikoa na wilaya za
jirani.
Duka hilo ni la sita kufunguliwa tangu Mhe. Rais Dk. John
Magufuli alipotoa agizo kwa MSD kufungua duka la dawa ndani ya Hospitali ya
Taifa ya Muhimbili, ambapo mengine yako katika mikoa ya Mwanza (Sekou Toure),
Arusha (Mount Meru), Mbeya (karibu na hospitali ya mkoa) na Geita (hospitali ya
wilaya ya Chato).
“Duka hili litasaidia kufikiwa kwa malengo ya Serikali ya
kuboresha huduma za afya kwa wananchi ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa dawa na
vifaa tiba kwa wakati na kwa gharama nafuu, hivyo nawaomba mlitumie duka hili,”
amesema.
Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuushukuru uongozi wa
benki ya NMB, kikosi cha SUMA JKT na MSD kwa kufanikisha ujenzi wa duka hilo
ambalo litaimarisha upatikanaji wa dawa kwa uharaka.
Awali Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu alisema
kuanzishwa kwa duka hilo kutaongeza upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwa
gharama nafuu , hivyo kuondoa usumbufu kwa wagonjwa wa kwenda kuzitafuta katika ya mbali na kwa
bei kubwa.
“Nitoe mfano wa tofauti wa bei za dawa kati ya maduka
yetu na mengine, dawa ya sindano ya diclofenac tunauza sh. 250 huku mitaani ni
sh. 1,000 hadi 1,500 , ampliclox dozi moja MSD sh. 1,500 mtaani sh. 3,500 na
Ciprofloxacin MSD sh. 100 na mtaani sh. 500 hadi 1,000,” amesema.
Mkurugenzi huyo amesema lengo la maduka hayo si kuuza
dawa reja reja, nia yao ni kuziuzia hospitali, vituo vya afya na Zahanati ili
wagonjwa wanapokwenda huko kupatiwa huduma wasikose dawa kwa wakati.
Akizungumzia kuhusu gharama za ujenzi wa duka hilo
Bwanakunu mesema umegharimu sh.milioni 59 ambapo kati yake MSD imetoa sh.
milioni 29 na benki ya NMB imetoa sh. milioni 30.
“Mbali na gharama za ujenzi MSD tumenunua na kufunga
vifaa vya TEHAMA kwa sh milioni 17 na mtaji wa dawa wa sh. milioni 37, ambapo
imetenga sh. milioni 100 kwa ajili ya dawa za duka hilo.
Amesema duka hili litaendeshwa na kusimamiwa na MSD kwa
muda wa mwaka mmoja na kisha wataikabidhi Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa
ajili ya kuliendeleza ambapo litaisaidia katika kuiongezea mapato.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAMOSI, JULAI 16, 2016
No comments:
Post a Comment