Rais wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi kesho Jumatatu,
Machi 13, 2017 anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye hafla ya kufunga kozi ya
ukocha ngazi ya ‘Intermidiate’ kwa makocha 27 wanaotarajiwa kuhitimu.
Kozi
hiyo iliyoendeshwa na Wilfred Kidao - Mkufunzi anayetambuliwa na Shirikisho la
Mpira wa Miguu Afrika (CAF), itafungwa saa 5.00 asubuhi kwenye Viwanja vya
Michezo vya Bandari, vilivyoko Tandika jijini Dar es Salaam.
Mbali
ya Kidao, wakufunzi wengine walikuwa ni Manyika Peter aliyefundisha programu au
mtaala kwa makocha wa makipa; Dk. Nassoro Ally Matunzya aliyewanoa makocha hao
kuhusu tiba za wanamichezo/wanasoka na Mkufunzi wa muda mrefu wa soka, Hemed
Mteza.
Wanafunzi
wa kozi hiyo wanaotarajiwa kuhitimu kesho Jumatatu ni pamoja Doris Malyaga
ambaye ni Mwanamke pekee kati ya wanafunzi 27 walisoma kozi hiyo kwa kipindi cha
siku 14 cha mwanzo wa mwaka. Doris ni mwanahabari za michezo aliyehudhuria kozi
hiyo. Anaandikia gazeti la MwanaSPOTI linalotolewa na Kampuni ya Magazeti ya
Mwananchi (MCL).
Wengine
ni nyota wa zamani wa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania ‘Taifa Stars’
waliopata kuchezea klabu kongwe na kubwa nchini. Wanafunzi hao ni Boniface
Pawasa, Fred Mbuna, Innocent Haule, Herry Morris, Ivo Mapunda, Nizar Khalfan na
Mussa Hassan Mgosi.
Wengine
ni Omar Kapilima, Amosi Mgisa, Uhuru Mwambungu, Yussuf Macho, George Minja,
Haruna Adolf, Selemani Omari, Ally Ruvu, Masoud Selemani, Haji Mustapha,
Mhasham Khatib, Issa Ndunje, Salum Kapilima, Said Salum, Julio Elieza, Hassan
Mwakami, Rajab Mponda, Ally Mbonde na Evod Mchemba.
..…………………………………………………………………………........................
IMETOLEWA NA
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
No comments:
Post a Comment