HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 25, 2017

SSRA YAWAANDALIA SEMINA MAAFISA HABARI NA MAWASILIANO SERIKALINI

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi. Irene Isaka (katikati), akiwa katika dawati la mapokezi akimuhudumia mteja kwa sura ya furaha katika maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Bi. Irene Isaka (wa pili kulia), akimsikiliza mteja kwa makini. 
Mkurugenzi wa Tafiti, Tathimini na Sera akifafanunua baadhi ya mambo wakati wa semina ya hifadhi ya Jamii kwa maafisa Habari na mawasiliano serikalini. 
Mkurugenzi wa Uhusiano na Uhamasishaji wa SSRA, Bi. Sarah Kibonde, akiwasilisha mada kuhusu hali ya hifadhi ya jamii nchini wakati semina kwa maafisa Habari na mawasiliano serikalini.
Maafisa Habari na mawasiliano serikalini wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa SSRA baada semina ya hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na SSRA kama sehemu ya maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma. 
Mkuu wa Kitengo cha Elimu kwa umma na mawasiliano toka Mamlaka ya Elimu Tanzania Bi. Silvia Lupembe akitoa neno la shukrani wakati wa semina ya hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na SSRA. 
Mkurugenzi wa Manunuzi na Ugavi Bw. Emmanuel Urembo akiwa kwenye dawati la mapokezi akimuhudumia mgeni aliefika kwenye ofisi za SSRA maeneo ya Kinondoni Moroco. 
Mkurugenzi Mkuu wa SSRA Bi. Irene Isaka akiwa na Wafanyakazi wa Mamlaka hiyo kwenye moja ya vikao vilivyoandaliwa katika wiki ya utumishi wa umma lengo likiwa ni kusikiliza na kutatua changamoto zao. 
Baadhi ya Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini wakifuatilia semina ya hifadhi ya jamii iliyoandaliwa na SSRA kama sehemu ya maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma 2017.

No comments:

Post a Comment

Pages