Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Kissa Kasongwa (kulia), akipokea madawati na vifaa vya ujenzi kutoka kwa Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Cosmas Sadat, katika hafla iliyofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Mtonga. Benki hiyo ilitoa msaada wa madawati 100 na vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya Sh. Mil. 30. (Na Mpiga Picha Wetu).
NA MWANDISHI WETU
BENKI
ya NMB, katikati ya wiki imekabidhi msaada wa madawati, vifaa vya afya na vifaa
vya ujenzi yakiwemo mabati na mbao, kwa shule mbalimbali wilayani Korogwe na
Kilindi mkoani Tanga, vyote vikiwa na thamani ya Sh. Milioni 60.
Pamoja
na vifaa hivyo vya kupaulia, pia NMB imekabidhi madawati 200 kwaajili ya
kupunguza uhaba wa madawati katika shule za wilaya hizo mbili.
Shule
zilizofaidika na msaada huo kwa upande wa wilaya ya Korogwe ni Shule ya Msingi
Mtonga (madawati 100), Shule ya Sekondari Semkiwa (viti 50 na meza 50) na Shule
ya Msingi Kwasemangube mabati, kofia na misumari vyenye thamani ya Sh. Milioni 5.
Nyingine
ni pamoja na Shule ya Msingi Kwamngumi (mabati yenye thamani ya Sh. Milioni 5),
Shule ya Sekondari ya Wasichana Korogwe (mabati ya Sh. Milioni 5) na Shule ya
Msingi Kijungumoto ya Halmashauri ya Mji Korogwe (mabati ya Sh. Milioni 5).
Kwa
upande wa wilaya ya Kilindi, Shule ya Sekondari Kimbe imepata viti na meza 100,
Shule za msingi za Mafisa, Nkama na Songe, zimepata mabati yenye thamani ya Sh.
Milioni 20. Pia, NMB imetoa vifaa tiba kwa zahanati mbili kila moja Sh. Milioni
5 na vifaa vyote kuwa na gharama ya Sh. Milioni 30.
Akizungumza
wakati wa kupokea msaada huo, Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Kissa Kasongwa, aliishukuru
NMB kwa msaada huo wilayani kwake na kusema utawasaidia kukabiliana na
changamoto za uhaba wa madawati na vifaa vya ujenzi wa madarasa kwenye sekta ya
elimu.
Kasongwa
alisema pamoja na maendeleo makubwa yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano
kwenye Sekta ya Elimu kwa elimu bila malipo, bado ni muhimu wadau kuchangia elimu
ili kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo kwa sasa.
Kwa
upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Sauda Mtondoo, alisema vifaa tiba na
madawati walivyopewa na Benki ya NMB, vitasaidia kuboresha miundombinu ya shule
na kuboresha afya za wananchi.
Naye
Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Cosmas Sadat, alisema NMB imekuwa ikisaidia
miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi kwa kujikita zaidi kwenye elimu kwa
kutoa madawati na viti, huku kwenye sekta ya afya wakichangia vitanda, magodoro
na kusaidia majanga yanayoipata nchi yetu.
No comments:
Post a Comment