Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Fastjet Tanzania, Capt. Arif Jinnah(kulia) akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam leo kuhusu uteuzi mpya wa
Mwenyekiti Mpya wa Fastjet Tanzania Lawrence Masha. Pichani wengine ni
Mwenyekiti Mtendaji Mpya wa Fastjet Tanzania, Lawrence Masha na Mkuu wa Mahusiano ya Kiserikali wa Fastjet Tanzania, Eng. August Kowero.
Mwenyekiti Mtendaji Mpya wa Shirika la Ndege Fastjet Tanzania,
Lawrence Masha akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam
leo kuhusu uteuzi wake wa kuwa mwenyekiti wa shirika hilo. Pichani kulia
ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Fastjet Tanzania, Capt. Arif Jinnah na
kushoto ni Mkuu wa Mahusiano ya Kiserikali wa Fastjet Tanzania, Eng.
August Kowero.
NA MWANDISHI WETU
MWENYEKITI
Mtendaji mpya wa Shirika la Ndege la Fastjet Airlines Ltd, Tanzania, ameelezea
mikakati madhubuti ya kuendelea kuhudumia soko la ndani na nje ya nchi, ikiwa
kama kampuni inayomilikiwa na Watanzania pamoja na masoko ya talii za nje.
Novemba
6 mwaka huu, Fastjet ilimteua Lawrence Masha kuwa Mwenyekiti Mtendaji wa kwanza
wa shirika hilo, uteuzi ambao umethibitisha nia ya kimkakati ya Fastjet kuhudumia
soko la ndani na nje ya nchi kulingana na uwezo na pato la Mtanzania.
Akizungumza
jijini Dar es salaam jana, Masha alisema: “Tumejikita zaidi kwa Watanzania
ambao wamefaidika kutokana na huduma zetu kwa miaka sita sasa. Tunatarajia kuongeza
safari za ndani na pia kuongeza idadi ya ndege ambazo zinakidhi mahitaji ya
soko.
“Tunaona
fursa kufanya kazi na kushirikiana na mashirika ya ndege za ndani na nje ya
nchi pamoja na Air Tanzania kutimiza mikakati ya Serikati ya utalii,” alisema
Masha.
Imeelezwa
kuwa, kati ya mashirika ya ndege yanazokua kwa kasi zaidi, Fastjet Airlines
Ltd, Tanzania, ambayo imetoa huduma kwa miaka sita, ikiwa imesafirisha zaidi ya
abiria milioni 2.5 ndani ya Tanzania pekee.
Fastjet,
lenye bei nafuu, linahudumia usafiri wa ndege katika miji ya Dar es Salaam,
Mwanza, Mbeya, Kilimanjaro, Lusaka na Zimbabwe, ambako lina rekodi ya
kusafirisha wastani wa abiria 30,000 kwa mwezi.
No comments:
Post a Comment