HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 07, 2013

MANCHESTER UNITED KUADHIBIWA KWA UTOVU WA NIDHAMU


 Luis Nani wa Man United akimchezea rafu mbaya Alvaro Abeloa wakati wa mechi kati ya timu hiyo na Real Madrid
 Nani akioneshwa kadi nyekundu na mwamuzi Cuneyt Cakir wa Uturuki.
 Nani akishindwa kuamini kilichomkuta
 Sir Alex Ferguson akilala kwa mwamuzi wa akiba kutokana na kadi nyekundu aliyooneshwa Nani.
Wachezaji wa Man United wakimtangulia mwamuzi Cuneyt Cakir anayesindikizwa na askari polisi.

MONACO, Ufaransa

Kadi nyekundu ya Luis Nani iliwatibua nyongo Man United, ambapo ‘waliotoka’ mchezoni na kujikuta ikichapwa mabao 2-1 ilipowaalika Real Madrid, kabla ya Ferguson kususia mkutano na vyombo vya habari

KAMATI ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa), iko katika mpango wa kuiadhibu klabu ya Manchester United, kutokana na vinara hao wa Ligi Kuu ya England kuonesha utovu wa nidhamu wakati wa mechi ya kichapo kutoka kwa Real Madrid Jumanne Usiku.

Bodi hiyo yenye mamlaka ya kinidhamu katika shirikisho hilo, inapanga kuijadili kadi nyenkundu ya moja kwa moja aliyooneshwa Luis Nani, ikiwemo kususia mkutano na vyombo vya habari baada ya mechi uliofanyika ndani ya dimba la Old Trafford.

Nani, nyota wa kimataifa wa Ureno, alitolewa nje kwa kadi nyekundu na mwamuzi Mturuki Cuneyt Cakir kunako dakika ya 56 kwa kumkanyaga kifuani Alvaro Arbeloa wakati akiwania mpira.

Baada ya kadi hiyo iliyotoka wakati United ikiongoza kwa bao la kujifunga la Sergio Ramos, wenyeji hao wakapoteza dira na kujikuta ikichapwa mabao 2-1 na kutupwa nje ya michuano kwa jumla ya mabao 3-2.

Sasa kadi hiyo ya Nani itajadiliwa na kamati hiyo, kuweza kuona kama itakuwa ya kifungo cha mechi moja, ama watamuongezea adhabu ya kukosa mechi zaidi.

Kocha wa Man United, Sir Alex Ferguson alikasirishwa na kadi hiyo na kuamua kususia mkutano wake na vyombo vya habari, huku msaidizi wake Mike Phelan akichukua nafasi yake kuzungumza na waandishi.

Phelan alimtetea bosi wake kwa kusema hayuko katika akili ya kawaida kuweza kuzungumza na akiwa mkutanoni kwa niaba ya Mscochi huyo alisema: "Kuna taharuki kuu chumba cha kuvalia, hali kaadhalika kwa kocha, ndio maana mimi niko hapa."

Uefa imesema kamati husika itakutana kujadili na kutoa maamuzi juu ya yote yanayohusu mechi hiyo hapo Machi 21.

Haijulikani kama beki wa Mashetai Wekundu hao Rio Ferdinand, atakuwamo katika maamuzi ya kamati hiyo, baada ya mlinzi huyo kumshutumu vikali Cakir baada ya filimbi yake ya kumaliza mchezo, ambapo kundi la wachezaji wa United walimzonga mwamuzi huyo.

BBC Sport/The Sun

No comments:

Post a Comment

Pages