HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 17, 2013

MSUVA AIOKOA YANGA MKWAKWANI TANGA



TANGA, Tanzania

Mshambuliaji Simon Msuva wa klabu ya Mabingwa wa Soka Afrika Mashariki na Kati Yanga, leo ameendeleza mpango wake wa kufunga walau bao 1 katika kila mechi lala salama ya ligi kuu Tanzania Bara.

Msuva aliiambia Habari Mseto hivi karibuni kuwa, hatahakikisha mechi zote zilizobaki anafunga ili kuendeleza mikakati yake na malengo ambayo amejipangia katika ligi hii 2012/13 inayofikia ukingoni Mei 18 mwaka huu.

“Namshukuru mungu nilichokipanga katika mechi hizi zilizosalia kwa sasa nimekifanikisha hata leo katika mchezo wetu na Mgambo JKT nimefunga japokuwa tumetoka sare, ya bao 1-1 eheee mungu nisaidie,”amesema.

Mchezaji huyu aliyetua Yanga akitokea Moro United ilishuka daraja msimu uliopita, amekuwa mwiba katika timu yake na kuwapa presha baadhi ya washambuliaji katika timu hiyo yenye makazi yake mtaa wa Twiga na Jangwani Kariakoo jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages