HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 09, 2013

DIMITROV AMNG'OA DJOKOVIC MADRID OPEN 2013

Novak Djokovic akirudisha mpira kwa mpinzani wake Grigor Dimitrov (hayuko pichani, katika mechi ya raundi ya pili ya michuano ya Madrid Open 2013 juzi.


MADRID, Hispania

Dimitrov, anayekamata nafasi ya 28 ya ubora duniani, halikuwa hajawahi kushinda hata seti (achilia mbali mchezo) dhidi ya Djokovic katika mara mbili walizowahi kukutana, lakini juzi alikuwa kwenye kiwango cha juu na kushinda kwa 7-6 (8-6) 6-7 (8-10) 6-3

KINARA wa viwango vya dunia vya ubora katika mchezo wa tenisi, Novak Djokovic, juzi ameshangaza mashabiki wa mchezo huo kwa kukubali kichapo katika raundi ya pili ya Michuano ya Wazi ya Madrid ‘Madrid Open 2013’ dhidi ya Grigor Dimitrov.

Dimitrov, anayekamata nafasi ya 28 ya ubora duniani, halikuwa hajawahi kushinda hata seti (achilia mbali mchezo) dhidi ya Djokovic katika mara mbili walizowahi kukutana, lakini juzi alikuwa kwenye kiwango cha juu na kushinda kwa 7-6 (8-6) 6-7 (8-10) 6-3.

Nyota huyo wa kimataifa wa Bulgaria, mwenye miaka 21, alionekana kumkabili vema Djokovic katika mechi hiyo na licha ya kushindwa kupata ushindi katika seti ya pili, kila mmoja aliona umakini aliokuwa nao na kujua.

Akizungumzia ushindi huo, Dimitrov alisema: "Ulikuwa ushindi mikubwa kwangu mimi. Najua lilikuwa jambo kubwa, bila shaka, lakini unahitaji kukaa tayari mchezoni.

"Ni matumaini yangu kwamba unapaswa kujiweka tayari kukabiliana na nyota kama huyu kwa miaka yako mchezoni. Ndio mechi ilivyo. Huwezi kujua namna gani hali ya mambo itakuwa mnapokutana mara nyingine."

Djokovic, ambaye alitwaa taji la tatu kwa mwaka huu aliposhinda ubingwa wa Monte Carlo Masters mwezi uliopita, alilazimika kutibiwa jeraha la enka alilopata katikati ya seti ya pili ya mpambano huo.

BBC Sport

No comments:

Post a Comment

Pages