HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 29, 2013

NGWEA AFARIKI SIKU MOJA KABLA YA KUREJEA TANZANIA

Na Elizabeth John



TASNIA ya muziki wa Hip hop nchini, imepata pengo kubwa baada ya kumpoteza nyota wa muziki huo, Albert Mangwea ‘Ngwea’, aliyefariki juzi akiwa Afrika Kusini alipoenda kwaajili ya kufanya shoo.

Ngwea aliondoka nchini mwezi uliopita alialikwa kafanya shoo nchini humo ambayo aliifanya wiki tatu zilizopita, jana alitegemea kurejea nchini.

Kwa mujibu wa Arusha255 Blog, baba mdogo wa marehemu mzee Mangwea ambaye yuko Mbinga mjini Songea, amesema kuwa wamekubaliana na kaka yake mkubwa yaani baba mkubwa wa Ngwair, David Mangwea ambaye naye yuko Songea kuwa watu watakutanika Mbezi kwa msiba na pia mapokezi yatafanyika Dar es salaam Mbezi Beach.

Taarifa zinaeleza zaidi kuwa ingawa bado kikao cha familia nzima hakijafanyika lakini baba huyo mdogo amesema wanaweza kulazimika kuzika Morogoro sehemu ambayo baba yake alizikwa.
Baba mdogo wa marehemu alisema kuwa  tayari ndugu wameshaanza kufanya taratibu za kuwasiliana na Ubalozi wa Tanzania Afrika ya Kusini ili kujua ni jinsi gani mwili huo utafika hapa nyumbani.

Naye msanii wa muziki huo, Moses Bushagama ‘Mez B’ mwili wa marehemu ulikabidhiwa jana kwa Watanzania ambao wanaishi nchini humo.

“Bado hatujapata taarifa kamili kuhusu kuletwa kwa mwili wake, lakini leo (jana) wanaukabidhi kwa Watanzania ambao wapo huko, binafsi bado siamini kama ‘mshikaji’ ametutoka hadi niuone mwili wake,” alisema Mez B. 

Naye msanii wa muziki huo, Mbwana Mohammed ‘Mb Doggy’ alisema Ngwea alikua ni msanii bora nchini na hakuna atakayeweza kuziba pengo lake, tumuombee apumzike kwa amani.

“Kinachotakiwa ni kumuombea mwenzetu apumzike kwa amani hiyo ni mipango ya mungu, leo kwake kesho kwa mwingine,” alisema Mb Doggy.


Juhudi za kumtafuta rafiki yake wa karibu, ambaye pia ni msanii wa muziki huo, Khalid Mohamed ‘TID Mnyama’ ambaye alikua ni mtu wa mwisho kuongea nae ziligonga mwamba baada ya kusema hawezi kuzungumza lolote kuhusiana na msiba huo kwani bado haamini kama kilichotokea ni cha kweli.

No comments:

Post a Comment

Pages