HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 19, 2013

POLISI NA KASHFA RUSHWA

Na Mwandishi Wetu

BAADHI ya polisi wa Kituo kidogo cha Sitakishari Ukonga wailayani Ilala wanadaiwa kuacha kumfungulia jalada la kesi mwizi wa viroba 71vya unga wa sembe, kumjeruhi muuzaji wa duka la unga huo, baada ya kudaiwa kupokea rushwa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Victoria Mwasonya, alisema tukio hilo lilitoke kwenye duka la Mwera Super Sembe wiki iliyopita, Pugu Kaujiungeni (Kona).

Alisema mtu huyo (jina tunalo), alifika dukani hapo akiwa na gari ghafla alianza kumshambulia kijana aliyetajwa kwa jina moja la Jonas, mara baada ya kumjeruhi alipakiza unga huo na kuikimbia kusikojulikana hata hivyo baada ya taaria hizo kufika polisi mtu huyo alikamatwa.

Mwasonya alisema baada ya kufikishwa kituo cha Polisi Sitakishari, katika hali ya kushanaza  paoja PF3 kuonyehsa kuwa mtu huyo alimjeruhi vibaya Jonas bado askari hao walishindwa kumfungulia kesi, huku wakishindwa kutoa maelezo ya kuridhisha kwa husika.

“Kwanza mimi nashangaa hata lile gari lililohusika kubeba mifuko ya unga wa wizi wameliachia bila yakutueleza sasa tukifika mahakamani watambuwe kuwa nao ni wezi kwa kuwa wamemsaidia mwizi kubeba vile viroba kwani hangeweza kuvibeba pekee yake”alisema Mwsonya.

Mwasonya alisema anaushahidi wa jina la askari aliyemtaka atoe rushwa ili asaidiwe kupata haki yake, lakini alipokataa kufanya hivyo alitakiwa  aondoke kituoni hapo, pamoja na kijana wake wakati huo akiwa bado yuko hospitalini matokeo yake ni hayo.

Alipotafutwa mkuu wa kituo hicho (OCS), Mary Saria kulitolea ufafanuzi suala hilo alisema kuwa hangeweza kulizungumzia kwa kuwa wakati huo alikuwa kwenye daladala.

Naye Jonas ambaye ni mpelelezi wa tukio hilo alisema suala la jalada la mtuhumiwa huyo aulizwe mkubwa wake kwani yeye hana haki ya kulizungumzia hilo.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Marietha Minangi, alisema hajalipata tukio hilo bali aliomba mwandishi ampe namba ya mlalamikaji ili awasiliane naye kwa taarifa zaidi kitendo ambacho mwandishi alikitekeleza.

Hata hivyo, mwandishi alipomtafuta tena majira ya saa 8:15 mchana simu yake iliita bila kupokelewa wakati namba hiyo alipewa majira ya asubuhi. 

No comments:

Post a Comment

Pages