HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 11, 2013

YAYA TOURE KUIBEBESHA UBINGWA WA FA MAN CITY LEO?


LONDON, England

Aidha, Toure anaamini kuwa kustaafu ghafla kwa kocha Sir Alex Ferguson wa Manchester United, kutaingozea nguvu na kuibeba Man City katika msimu ujao wa Ligi Kuu na michuano ya ndani

MANCHESTER City leo inashuka kwenye Uwanja wa Wembley kuivaa Wigan katika fainali ya Kombe la FA, huku kiungo wake Yaya Toure (pichani kulia), akitamba kupania kuibebesha Man City ubingwa kama alivyofanya mwaka juzi.

Akizungumzia pambano hilo ambalo Man City inajiandaa kuthibitisha ubora wake kwa kutwaa taji la tatu katika miaka mitatu, Toure alisema alisaini mkataba wa kuichezea klabu hiyo ili kuwa sehemu ya historia ya klabu hiyo na nafasi hiyo ataitumia vema.

“Kila mwaka ni muhimu kwa klabu kwa sababu tunataka hii kuifanya kuwa moja ya klabu kubwa. 

Tumelitema taji la Ligi Kuu kwenda kwa mahasimu wetu Man United, lakini sasa tutaka kutwaa ubingwa huu.
“Tunatakiwa lazima tutwae ubingwa, hiyo ndio sababu ya mimi kusaini mkataba mpya. Nataka kuwa sehemu ya historia ya klabu hii.

“Tayari tumelianza hilo, kwa kuwa tumeshaanza kutwaa baadhi ya mataji.

“Nina matumaini kwamba kuna mengine zaidi yanakuja hapa, kama vile Ligi ya Mabingwa Ulaya, Ligi Kuu na Kombe la FA,” aliongeza Toure.

Toure, 29, alikuwa shujaa wa Man City miaka miwili iliyopita ndani ya Uwanja wa  Wembley, ambako alifunga mabao mawili moja katika nusu fainali dhidi ya Man United na jingine kwenye fainali dhidi ya Stoke City.

Kiungo huyo alisema: “Hiyo ilikuwa moja ya fainali za aina yake kwangu mimi. Nilifanya mashambulizi na kufunga na kwa sababu hiyo nikapeleka medali ya ubingwa Etihad na kwa mashabiki kwa ujumla.

“Hilo lilikuwa jambo muhimu ambalo tulikuja hapa kwa ajili ya kupata mafanikio,” alitamba Toure.

Aidha, Toure anaamini kuwa kustaafu ghafla kwa kocha Sir Alex Ferguson wa Manchester United anayerithiwa na David Moyes, kutaingozea nguvu na kuibeba Man City katika msimu ujao wa Ligi Kuu na michuano ya ndani.

Man City ambao wamekuwa wapinzani wa karibu wa Man United katika miaka miwili sasa ya ligi hiyo, wanahisi nguvu ya United itakuwa imepungua kwa kuondoka Ferguson Old Trafford.

“Man United ni klabu kubwa na Ferguson ni mbobevu aliyeleta mafanikio pale. Amejenga kila kitu ndani ya United na uwiano, ninatumaini, hamasa itakwenda upande wa Man City kwa sasa.

“Tutaona msimu ujao. Kutakuwa na upinzani mkubwa kati ya Chelsea, Liverpool, Arsenal na Man United. Tottenham nayo inakuja kwa kasi na ni wazi kutakuwa na Ligi Kuu ngumu mno.”

The Sun 

No comments:

Post a Comment

Pages