HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 27, 2013

NUSU FAINALI KOMBE LA MABARA 2013: NI HISPANIA VS ITALIA LEO

Kiungo Cesc Fabregas wa Hispania kushoto, akitafuta mbinu za kumtoka Andrea Pirlo wa Italia katika fainali ya Euro 2012

RIO DE JANEIRO, Brazil 

Baada ya jana kushuhudia mchuano wa miamba ya Amerika Kusini Brazil dhidi ya Uruguay, ulioisha kwa Brazil kuichapa Uruguay mabao 2-1, leo michuano hiyo inaendelea kwa Hispania kuivaa Italia, zote zikipewa nafasi sawa ya kutinga fainali ya michuano hiyo iliyoanza Juni 15 na itafikia tamati Jumapili Juni 30

MIAMBA ya soka barani Ulaya, timu za taifa za Italia na Hispania, leo zinajitupa kwenye dimba la Estadio Castelao, jijini Fortaleza, katika pambano kali la nusu fainali ya pili ya Kombe la Mabara 2013 inayoendelea nchini hapa.

Baada ya jana kushuhudia mchuano wa miamba ya Amerika Kusini Brazil dhidi ya Uruguay, ulioisha kwa Brazil kuichapa Uruguay mabao 2-1, leo michuano hiyo inaendelea kwa Hispania kuivaa Italia, zote zikipewa nafasi sawa ya kutinga fainali ya michuano hiyo iliyoanza Juni 15 na itafikia tamati Jumapili Juni 30.

Nusu fainali hii ni marejeo ya miamba hiyo, iliyoumana katika fainali ya Mataifa Ulaya ‘Euro 2012,’ iliyopigwa Julai 1, 2012 kwenye dimba la Olimpiki jijini Kiev, Ukraine, ambako Hispania iliichapa Italia kwa mabao 4-0.

Wakati Italia ikifuzu hatua hii bada ya kushika nafasi ya pili katika kundi A nyuma ya Brazil, Hispania imefuzu kama kinara wa Kundi B, ikifuatiwa na Uruguay baada ya mechi tatu tatu za hatua ya makundi.

Safu ya ushambuliaji ya Hispania imeonesha uhatari, baada ya kutikisa nyavu mara 15 huku mabeki wake wakiruhusu bao moja tu, katika mechi zake tatu za ushindi.

Kwa upande wa Azzurri, licha ya washambuliaji wake kutisha kwa kufunga mabao nane katika mechi tatu – ilikoshinda mbili na kufungwa moja, safu ya ulizni ya kikosi hicho imeonesha udhaifu, baada ya kuruhusu mabao nane pia katika mechi hizo.

Washindi wa nusu fainali ya jana na leo, wataumana katika fainali kali Juni 30 kwenye dimba la Estádio do Maracanã, jijini hapa, kuwania kitita cha dola za Kimarekani milioni 4.1, huku mshindi wa pili akilamba dola milioni 3.6.

Aidha, timu zitakazofungwa katika hatua hii zitaumana mapema Juni 30 hiyo hiyo kwenye Uwanja wa Arena Fonte Nova, jijini Salvador, kuwania zawadi ya tatu ya dola milioni 3, huku mshindi wa nne akiambulia dola milioni 2.5.

Kabla ya nusu fainali ya kwanza jana usiku, mshambuliaji Fernando Torres wa Chelsea, alikuwa akiongoza mbio za Kiatu cha Dhahabu cha michuano hiyo ya kwanza kabisa kutumia Teknolojia ya Goli (Goal Line Technology - GLT), akiwa na mabao matano.

Supersport.com

No comments:

Post a Comment

Pages