HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 20, 2013

CHADEMA yamtaka Waziri Makala asikumbatie watuhumiwa wa Ufisadi

Na Bryceson Mathias, Mvomero
DIWANi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kata ya Nyandira  wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro, amemtaka Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makala, asiwakumbatie watuhumiwa wa Ufisadi wa zaidi ya Mil. 10/- za Minara ya Simu ya kijiji hicho.
Diwani wa CHADEMA kata hiyo, Peter Zengwe amesema Makala amepokea kuwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na viongozi wa chama hicho wilaya, wamewapokea aliyekuwa Mwenyekiti, Yodosi Msimbe, na aliyekuwa Mtendaji Elnestina Mponda.
 Zengwe alitoa Kauli hiyo mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa Makala uliofanyika katika kijiji cha Nyandira Augosti 19, na kuhutubiwa na Naibu Waziri huyo.
,”Makala katika hali iliyowashangaza wananchi, aliwapokea kiwepesi sana watuhumiwa hao kuwa wanachama wa CCM, ilihali anajua Chadema kimekuwa kikirumbana nao baada ya kuwabaini kuhusika na tuhuma hizo na kuwashitaki Polisi toka 2008.
“Kwa kuogopa Ukali wa Chadema, watuhumiwa hao wameona wakimbilie CCM maana huko ndiko kunakowafuga watuhumiwa na kuwakumbatia, maana Wimbo wa Chadema M4C, hawauwezi ”. Alisema Zengwe.
Katika mkutano huo, Makala aliongozana na Mhandisi wa Wilaya aliyejulikana kwa jina Moja la Jacob, ambaye imedaiwa alikwenda kwa lengo la kutoa amri ili Jengo la Chadema lililojengwa na Zengwe, zilizvunjwe, madai limejengwa chini ya kiwango, jambo ambalo alikanusha..
Awali wanachama hao walitangaza kujiunga na Chadema,lakini baada ya kubanwa ili watoe maelezo kuhusiana na tuhuma zinazowakabiri, waliamua kurejea CCM waliokotoka, na waziri Makala kuwapokea kwenye mkutano huo

No comments:

Post a Comment

Pages