HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 20, 2013

Rasimu ya Katiba; Dk. Slaa awageukia Viongozi wa Dini

Wanafunzi wakiishangaa helkopta ya Dk. Wilbroad Slaa ikishuka katika Uwanja wa Wajenzi Dodoma.

Na Bryceson Mathias, Dodoma
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, jana Juni 19, 2013 katika viwanja vya Wajennzi Dodoma, amewageukia Viongozi wa Dini nchini akiwataka wakiwa Madhabahuni na kugeukia Kibra, wajikite kuhubiri Haki ya Watanzania.
Mbali ya usia huo, Dk. Slaa pia aliwauliza wananchi wa Dodoma Swali Gumu iwapo Vyama na wao nani alianza kuwepo mkoani Dodoma, Je ni Vyama au Wananchi? Wakajibu wao, akaonya TANU, UNIP,vilikuwepo vikafa; hivyo wasikubali kuburuzwa na Vyama.
Akizungumzia Rasimu ya Katiba baada ya Mwanasheria wa Chadema Edson Mbogolo kutoa Elimu ya Mabadiliko ya Katiba yanayoungwa Mkono na Chadema na yale yanayokataliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), ambapo Slaa alishangaa nchi kuwa na Amiri Jeshi Wakuu Wawili.
“Hakuna Mtanzania asiyemfahamu Jaji Joseph Sinde Warioba, ni Jaji na alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alimwamini akamchagua awe Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya. Leo ametoa mapendekezo CCM ajabu wanayapinga.
“Wapinzani tunaaminika tunapinga kila Kitu, ila mapendekezo ya Jaji Warioba tumeyakubali asilimia kubwa kwa sababu inaeleza mustakabali Uchumi wa Taifa na Rasilimali za Vizazi Vyetu, Tunu za Taifa, Malengo Makuu, Uwazi, Utu, nauliza, CCM na Chadema nani Mpinzani?”..wananchi CCM!.
Slaa alisema, Rasimu imeeleza Serikali ilinde Amani Uchumi iondoe Umaskini, Izuie Vitisho, Ubaguzi, Rushwa,Uonevu, Dhuluma,Unyanyasaji na Utajiri utumike kwa wote na mengi mengine, lakini CCM inapinga yote hayo, Je Chadema na wo nani anamtetea Mwananchi?
“Twiga wanasafirishwa kwenye ndege, Meno ya Tembo kwenye Meli tena za Viongozi wa CCM walinzi wa Usalama wote wa ndani na Mipakani wapo, hoja ya kuwadhibiti waharifu hao inapingwa, si wanataka wakifanya hivyo sheria isiwakamate?”.alisema Slaa na kushangiliwa.
Aidha wananchi walitoa maoni ikiwa ni pamoja na kufutwa kwa wakuu wa wilaya na Mikoa, wanaolipwa Mil.11/-, Rais ashitakiwe anapofanya makosa, Wawekezaji wawekeze kwa masharti ya Watanzania, Tume huru, IGP, Spika asitokane na Chama, Mawaziri wasiwe Wabunge, IGP athibitishwe na Bunge, na kwamba gharama za Serikali Tatu ni ndogo.

No comments:

Post a Comment

Pages