HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 16, 2013

AZAM MEDIA WAZINDUA MAKAO MAKUU YA AZAM TVMkurugenzi Mtendaji wa Azam Media, Yusuf Bakhresa akisalimiana na wasanii wakati wa ufunguzi wa Ofisi ya AZAM TV.Baadhi ya wasanii maarufu nchini wakiwa na Meneja wa Uhusiano wa AzamTV, Maryam El-haj  wakati wa ufunguzi wa Ofisi ya AZAM TV. 



DAR ES SALAAM, Tanzania

WASANII wa filamu nchini, wamekiri kufurahishwa kwao na ujio wa kituo cha Teevisheni cha Azam (Azam Tv) na kuutaja kama ukombozi utakaochagiza maendeleo ya sanaa na wasanii ndani na nje ya nchi.

Wakizungumza wakati wa uzinduzi wa Makao Makuu ya Kampuni ya Azam Media Ltd, wasanii hao, Jacob Steven ‘JB’, Mahsen Awadh ‘Dk Cheni’, Yvone Cherry ‘Monalisa’ na Suzan Lewis ‘Natasha,’ walisema kama wasanii wanatarajia mengi yaliyo bora kutoka Azam Tv.

Kwa upande wake JB alisema sanaa ya Tanzania hususani ya filamu na wadau wake, wamepata sehemu muhimu itakayosaidia kukuza sio tu kiwango cha ubora wa kazi zao, bali pia pato la wasanii kutokana kutokana na mikataba ya matangazo ya muvi zao.

“Tuna matumaini makubwa kwamba ujio wa Azam Tv ni moja ya njia zitakazoboresha kazi na pato la wasanii. Ni fursa nyingine ambayo wasanii tunapaswa kuitumia vema ili kuwafikia wadau wetu kupitia,” alisema JB mmoja wa wasanii nguli wa Bongo Muvi.

Monalisa, yeye alibanisha kuwa matarajio ya wasanii wengi ni kuwa ujio huo wa Azam Tv utakwenda sambamba la ongezeko la mikataba ya kurushwa kwa filamu zao, kwani kabla ya hapo kulikuwa na mikataba michache.

“Naamini hii ni moja ya neema miongoni mwa wasanii, lakini kwa sanaa na wadau wake kwa ujumla. Tutapata mikataba minono ya kurushwa kwa filamu zetu hapa na kutanua pato letu. Hakika nimefurahia ujio wa Azam Tv,” alisema Monalisa.

Dk Cheni naye hakuwa mbali na maoni ya wenzake, akisema anaamini fursa ya wasanii kuwafikia wadau na wadau kupata vilivyo bora kutoka kwao imepata kiunganishi muhimu ambacho ni Azam Tv.
“Kwangu mimi Azam Tv ni zaidi ya kituo cha Televisheni. Nakichukulia hiki kama kiunganishi muhimu cha sisi kuwafikia mashabiki wetu, lakini wao pia kutuona kwa mapana na kuchangia maendeleo ya sanaa na wasanii Tanzania,” alisema Dk Cheni.

Natasha yeye kwa upande wake aliupongeza uongozi wa Azam Media kwa kuwajali wasanii kwa kuanzisha chaneli ya Sinema Zetu inayopatikana katika king’amuzi cha Azam Tv na kwamba anaamini itakuwa chachu kuu ya mafanikio ya sanaa nchini. 

No comments:

Post a Comment

Pages