HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 18, 2013

TANZANIA DISTILLERIES  LIMITED (TDL) YAZINDUA PROMOSHENI YA AMARULA
Meneja wa kinywaji cha Amarula kutoka Kampuni ya Konyagi Tanzania, Diana Baliagati (katikati), Meneja Mauzo wa Kanda, Mwesige Mchuruza (kushoto) na Meneja wa Shoprite, Venans Matias wakizindua promosheni ya kinywaji hicho  jijini Dar es Salaam. Mshindi wa promosheni hiyo atapata fursa ya kwenda Afrika kusini na rafiki yake kwenda kushuhudia shamba na utengenezaji wa kinywaji hicho.

DAR ES SALAAM, Tanzania

KAMPUNI ya  Tanzania Distilleries Limited (TDL) leo imetangaza promosheni ya shindano la kumsaka mshindi wa anayetumia kinywaji cha Amarula, kinacho tengenezwa nchini Afrika Kusini na kusambazwa na TDL nchini maarufu kama nyumba ya Konyagi katika promosheni iliyozinduliwa leo Shoprite Mlimani City jijini Dar es Salam ijulikanayo kama  Amarula Pan Africa Promotion”.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Bidhaa wa TDL, Diana Baliagati alisema shindano hili la kumsaka mtumiaji wa Amarula litaanza rasmiDesemba 16,2013 hadi Januari 14, 2014.

Diana alisema lengo hasa ikiwa ni kuwapa fursa wanywaji wa Amarula kwenda kutembelea nchi ya Afrika Kusini na kushuhudua shamba la Amarula na kujionea matunda ambayo hutumika kutengenezea kinywaji cha Amarula.

Mshindi katika shindano hili,atapata tiketi moja itakayomuwezesha kusafari na mwenzake kwa ajili ya kwenda kushuhudia shamba la AMARULA,nchini Afrika Kusini na kufikia katika Hoteli ya nyota tano(5Star), alisema Diana.

Meneja bidhaa wa TDL, Diana Baliagati alisema, ili kupata nafasi ya kujishindia tiketi,mshiriki anapashwa kujaza kuponi zilizo katika shingo ya chupa kubwa za Amarula zinazouzwa katika maduka makubwa yote ya Shopritehusika.Chupa hizo za shindano la Amarula Pan Africa Promotionzitakuwa zikipatika kwenye maduka ya Shoprite tu.

Mshindi wa Amarula Pan Africa Promotion atapatikana  kupitia drooitakayofanyika Januari 14,2014, na safari itakuwa mwezi Februari.Mshindi atapewa taarifa zote zinazohusika na safarihiyo mara baada ya droo kufanyika.

No comments:

Post a Comment

Pages