HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 07, 2014

MEZ B ANUSURIKA KUUAWA


Na Elizabeth John
MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Moses Bushamaga ‘Mez B’ usiku wa kuamkia Jumamaosi alinusurika kuuwawa baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana, maeneo ya Sinza Vatcan jijini Dar es Salaam.

Akizungumza  jijini Dar es Salaam jana baada ya kutoka hospitali, Mez B alisema alivamiwa na watu asiowafahamu akiwepo baunsa ambaye alimuelekeza cha kufanya mtu huyo ambaye alimjeruhi vibaya maeneo ya usoni.

“Nilitoka kwa Noorah nilipofika maeneo ya White Inn, Sinza nikashuka kwenye gari baada ya hapo nikamuona baunsa anakuja mbele yangu alikuwa na jamaa mmoja hivi, huyo baunsa akamwambi yule jamaa fanya kazi yako, huyo jamaa akatoa kisu na kuanza kunijeruhi maeneo ya usoni yani hapa sitamaniki kabisa lakini nashukuru mungu bado napumua,” alisema Mez B.

Alisema wakati yeye anafanyiwa unyama huo, walinzi wa hapo walimuangalia tu hawakutoa msaada wa aina yoyote mpaka yule jamaa alipoacha mwenyewe kumfanyia unyama huo.

Mez B ni kati ya wasanii ambao wanatikisa katika muziki wa bongo flava, kutoka kundi la Chember Squared ambalo lilikuwa likiongozwa na mkali wa free style, marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ ma msanii Athuman Kapongo ‘Dark Master’.

Msanii huyo alishawahi kutamba na ngoma zake kama ‘Kikukuu cha Mama Rhoda’, ‘Kidela’ na ‘Kama Vipi’ ambao alishirikiana na mwanadada Rehema Chalamila ‘Ray C’ kabla hajapotea katika soko la muziki huo.

No comments:

Post a Comment

Pages