HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 27, 2014

NSSF YAFUTURISHA WASTAAFU NA WADAU WAKE MKOA WA TANGA

Principle Operation Officer wa NSSF, Joyce Mruma akigawa zawadi kwa wastaafu wa NSSF wakati wa hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na shirika hilo. 
Ofisa Mwandamizi wa Operesheni wa NSSF, Lydia Ignace akitoa zawadi kwa wastaafu wa Shirika hilo waliohudhuria hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na NSSF kwa ajili ya wastaafu wa Mkoa wa Tanga.
Principle Operation Officer wa NSSF, Joyce Mruma akitoa zawadi kwa mstaafu wa NSSF, Bella Antao wakati wa hafla ya kufuturisha wastaafu wa Shirika hilo.
Kaimu Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mkoa wa Tanga, Emmanuel Masika akizungumza wakati wa hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa kwa ajili ya wastaafu wa Mkoa wa Tanga.
Baadhi ya maofisa wa NSSF wakiwa katika picha ya pamoja.
Wastaafu.
Baadhi ya wastaafu wa NSSF Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kufuturisha wastaafu hao iliyoandaliwa na NSSF.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Ummy Mwalimu akizungumza katika hafla hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego akizungumza wakati wa hafla ya kufuturisha wastaafu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), iliyofanyika mkoani Tanga.
Sheikh Mkuu Mkoa wa Tanga, Alhaji Juma Luhudu akizungumza wakati wa hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na NSSF kwa ajili ya wastaafu wa Mkoa wa Tanga pamoja na wadau wake.
Mmoja wa wastaafu akitaka ufafanuzi kutika kwa viongozi wa shirika hilo kuhusu huduma za shirika hilo.
Mstaafu wa NSSF, Edith Lumeya akiuliza swali kuhusu malipo ya wastaafu.
Mstaafu wa NSSF, Muni Hussein Ally  akiuliza swali.
Meneja wa Mafao wa NSSF, James Oigo akijibu maswali ya baadhi ya wastaafu waliotaka ufafanuzi kuhusu huduma mbalimbali za shirika hilo. 
Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji, Maryam Muhaji hafla ya kufuturisha wastaafu iliyofanyika Mkoa wa Tanga. 
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Alhaji Juma Luwuchu akizungumza wakati wa hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na NSSF kwa ajili ya wastaafu wa Mkoa wa Tanga.
Baadhi ya wastaafu wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego (katikati).
Baadhi ya wastaafu wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego (katikati).
Baadhi ya Maofisa wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego (katikati), wa pili kushoto ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Alhaji Juma Luwuchu, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Chiku Matesa (wa  tatu kushoto), Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji, Maryam Muhaji.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Ummy Mwalimu, (kushoto)  akishiriki futari.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego (wa pili kushoto)  akiwaongoza akinamama kupata futari.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego (wa tatu kushoto), akishiriki katika futari iliyoandaliwa na NSSF kwa ajili ya wastaafu wa Mkoa wa Tanga pamoja na wadau wake. Kushoto ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Ummy Mwalimu na wa pili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa NSSF, Chiku Matesa.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego (kulia), akishiriki katika futari iliyoandaliwa na NSSF kwa ajili ya wastaafu wa Mkoa wa Tanga pamoja na wadau wake. Kushoto ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Ummy Mwalimu na Kaimu Mkurugenzi wa NSSF, Chiku Matesa.
Wastaafu na wadau wa NSSF Mkoani Tanga wakijumuika katika futari.
Waastaafu wa wadau wa NSSF Mkoani Tanga wakijumuika katika futari.
Wastaafu na wadau wa NSSF Mkoani Tanga wakijumuika katika futari.
Baaadhi ya wadau wa mfuko huo wakipata futari.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Chiku Matesa akiwashukuru Wastaafu na Wadau waliohudhulia futari iliyoandaliwaa na mfuko huo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Chiku Matesa akiwashukuru Wastaafu na Wadau waliohudhulia futari iliyoandaliwaa na mfuko huo.
Watoto wanaoishi katika Kituo cha Kulelea Watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Barabara ya 7 Mkoani Tanga wakiwa ni miongoni mwa wageni waalikwa katika futari iliyoandaliwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwa ajili ya Wastaafu na Wadau wa Mfuko huo iliofanyika mkoani Tanga.
Watoto wanaoishi katika Kituo cha Kulelea Watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Barabara ya 7 Mkoani Tanga wakiwa ni miongoni mwa wageni waalikwa katika futari iliyoandaliwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwa ajili ya Wastaafu na Wadau wa Mfuko huo iliofanyika mkoani Tanga.
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Alhaji Juma Luwuchu akiomba dua.

Na Elizabeth Kilindi, Tanga

SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limejipanga kuhakikisha linaboresha mfuko huo kwa kuwafikia wakulima na wafugaji nchini kote ili kupanua wigo kwa wanachama wake.

Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Chiku Matesa, wakati akizungumza katika hafla ya kufuturisha wastaafu (PENSHENI) pamoja na wadau wa mfuko huo iliyofanyika katika hotel ya Tanga Beach Resort Mkoani Tanga.

Alisema kuwa  wakulima na wafugaji wamekuwa wakisaulika hivyo kama shirika limeona vema kuwafikia ikiwemo kuwapatia elimu ambayo itawasaidia kujiunga na mfuko huo.

‘Sisi  kama shirika tumeona itakuwa ni vizuri zaidi kuwafikia wakulima na wafugaji ili kuweza kujiunga na mfuko wetu ambao unamafao uzazi, kuumia kazini, Kustaafu na mengineyo'.

Kaimu Mkurugenzi huyo alisema shirika limeanzisha mpango wa kutoa mikopo kwa wanachama wake kupitia Saccos ambapo utalenga kuwawezesha wanachama wa mfuko  huo kujikwamua kiuchumi.

Naye  Mkuu wa Wilaya Tanga Halima Dendego aliwataka  wafanyakazi waliojiajiri na walioajiriwa ikiwemo wa mashambani kujiunga na mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF ili kuweza kujiwekea akiba hasa ya uzeeni.


“Nawaasa hawa wafanyakazi wajiunge na mfuko huu kwani unafaida kubwa hasa unapostaafu unakuwa na uhakika wa kuishi maisha bora yasiokuwa na wasiwasi’’alisema Dendego. 

No comments:

Post a Comment

Pages