HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 26, 2014

BENKI YA CRDB YALETA UFANISI KATI YA WAFANYABIASHARA, WAWEKEZAJI WA CHINA NA TANZANIA

 Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB anayeshughulika na huduma ya China Deski, Ibrahim Masahi (kulia), akitoa ufafanuzi kuhusu huduma maalum za kibenki kwa ajili ya kusaidia wafanyabiashara na wawekezaji wa China na Tanzania, wakati wa maonyesho ya bidhaa za China yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. 
 Baadhi ya wateja wakisoma vipeperushi vyenye taarifa muhimu za Benki ya CRDB kuhusu huduma maalum ya China Deski.
 Baadhi ya watu waliofika katika banda la CRDB wakati wa maonyesho ya bidhaa za China wakisoma vipeperushi vyenye taarifa muhimu kuhusu huduma maalum ya China Deski.
 Ibrahim Masahi akitoa ufafanuzi kwa wateja waliotaka kujua huduma za China Deski.
Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB anayeshughulika na huduma ya China Deski, Ibrahim Masahi akizungumza na waandishi wa habari kuhusu huduma maalum za kibenki kwa ajili ya kusaidia wafanyabiashara na wawekezaji wa China na Tanzania, wakati wa maonyesho ya bidhaa za China yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
  
BENKI ya CRDB, imeeleza kupata faida baada ya kuanzisha deski la China kwa kuwaunganisha wafanyabiashara na wawekezaji kutoka China na hapa nchini.

Akizungumza jana katika maonyesho ya bidhaa za China Afrika, yanayofanyika jijini Dar es salaam, Meneja Uhusiano wa Deski hilo, Ibrahim Masahi, alisema kuwa huduma hiyo imerahisisha na kuwasaidia wafanyabiashara kupata mikopo na kufanya huduma za kibenki, kukuza wigo wa kibiashara.

Masahi alisema kuwa huduma hiyo umuwezesha mteja wa CRDB kutoa hadi kiasi cha sh milioni 40 kwa siku ikiwa atakuwa nchini China au Tanzania kwaajili ya biashara na kuwekeza.

“Tangu kuanza kwa hudyma hii benki kupitia deski la China imepata faida ya zaidi ya Bilioni 30, na imeunganisha wateja mbalimbali na wawekezaji wanaonunua bidhaa china, lakini kwa upande wa Tanzania Chnagmoto kubwa ni lugha wakiwa kule China na rate imekuwa ikibadilikabadilika,”alisema. 

Aidha aliwataka watanzania kuchangamikia fursa hiyo ambayo imeondoa madhara ambayo yangeweza kutokea na kueleza kuwa kwasasa wameingia ubia na benki zaidi ya 10 nchini China.

No comments:

Post a Comment

Pages