HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 11, 2014

FLAVIANA MATATA, PSPF WATOA MABEGI KWA WANAFUNZI 650 WA SHULE KATIKA HALMASHAURI ZA LINDI NA NACHINGWEA MKOANI LINDI

Mwanamitindo Flaviana Matata (wa tatu kutoka kulia waliosimama nyuma) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule ya  Msingi Mnengulo mkoani Lindi. Jumla ya wanafunzi 650 wa shule zilizipo katika  Halmashauri za Lindi na Nachingwea  mkoa wa Lindi wamenufaika na msaada huo wa mabegi hayo yenye vifaa mbalimbali vya shule, msaada huo umetolewa kwa pamoja kati ya PSPF na Taasisi ya Flaviana Matata. Kushoto ni  Meneja Mawasiliano, Masoko na Uenezi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Costantina Martin.


Na Mwandishi Wetu, Lindi

Mfuko wa Pensheni wa PSPF kwa kushirikiana na Taasisi ya Flaviana Matata imetoa msaada wa vifaa vya shule kwa wanafunzi walio katika mazingira magumu mkoani Lindi.

Flaviana Matata ambaye ni mwanamitindo anayefanya nchini Marekani amekabidhi mabegi 650, kila begi lina vifaa mbalimbali vya shule. 

Vifaa vilikabidhiwa na Flaviana Matata mwenyewe kwa baadhi ya wanafunzi  wa wilaya za Nachingwea na Lindi Mjini
Lengo la msaada huo ambao umetolewa kwa pamoja kati ya Taasisi ya Flaviana Matata na PSPF ni kuunga mkono juhudi za serikali za kuhakikisha kila mwanafunzi nchini Tanzania anapata elimu akiwa na vifaa muhimu vinavyohitajika.

Hii  ni mara ya pili kwa PSPF kwa kushirikiana na Taasisi ya Flaviana Matata kutoa msaada huo kwa wanafunzi, mwaka jana wanafunzi  wa shule mbalimbali mkoani Pwani walifaidika na msaada huo.

Mfuko wa Pensheni wa PSPF umekuwa ukijihusisha katika kusaidia maeneo mbalimbali yanayohitaji msaada ambao utaleta mabadiliko chanya kwa jamii ya Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Pages