HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 02, 2014

Watanzania waaswa kushiriki katika kuendeleza Sekta ya Elimu nchini

 SR1a:  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na M,ichezo Profesa Elisante Ole Gabriel akipokea zawadi ya maua kutoka kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi na Awali Sunrise ya jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya Saba ya wahitimu wa Darasa la Saba.
 Mwanafunzi anayehitimu Darasa la Saba katika Shule ya Msingi na Awali Sunrise Bw. Mark Ngalo akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wenzake wakati wa mahafali yao yaliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.Aliyemshikia kipaza sauti ni  Lulu Benson.
SR1b. Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi na Awali Sunrise ya jijini Dar es Salaam akito neno la kuwakaribisha wageni waliohudhuria mahafali ya wanafunzi wanaomaliza Darasa la Saba katika shule hiyo jijini Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na M,ichezo Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza na wazazi na wanafunzi wakati wa mahafali ya wahitimu wa Darasa la Saba wa Shule ya Msingi na Awali Sunrise ya jijini Dar es Salaam alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali  hayo.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na M,ichezo Profesa Elisante Ole Gabriel akimkabidhi Cheti mmoja wa wahitimu wa Darasa la Saba katika Shule ya Msingi na Awali Sunrise ya jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya Saba ya Shule hiyo yalifanyka jana jijini Dar es Salaam. Katika ni Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Onesmo Vitalis.
 Kikundi cha Skauti cha Shule ya Msingi na Awali Sunrise wakitoheshi mbele ya mgeni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel (hayupo pichana) alipokuwa mgeni rasmi katika mahafa ya saba kwa wahitimu wa Darasa la Saba katika shule hiyo jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi na Awali ya Sunrise  wakifurahia kwa michezo wa sanamu wakati mahafali ya darasa la Saba jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wahitimu wa Darasa la Saba wa Shule ya Msingi na Awali Sunrise ya jijini Dar es Salaam wakiwa wenye nyuso za furaha wakati wa mahafali yao.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na M,ichezo Profesa Elisante Ole Gabriel (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu wa Darasa la Saba wa Shule ya Msingi na Awali Sunrise ya jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya Saba ya hiyo. Picha zote na Frank Shija Afisa Mawasiliano Serikalini, WHVUM.


Na Rose Masaka, MAELEZO

Watanzania waaswa kuheshimu na jitihada za kukuza na kuendeleza Elimu zinazofanywa na wadau mbalimbali hapa nchi zikiwemo sekta binafsi ambapo amesma sekta hii muhimu ndiyo chimbuka la maadili mema kwa Taifa.

Rai hiyo imetolewa na Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa  Elisante Ole Gabriel wakati akizungumza na wanafunzi na wageni mbalimbali katika mahafali ya Darasa la Saba wa Shule ya Msingi na Awali Sunrise jana jijini Dar es Salaam.

Profesa Elisante alisema kwamba Elimu ni suala mtambuka ambapo kila mwananchi mwenye mapenzi mema na nchi yake ana wajibu wa kuenzi na kusaidia katika jitihada za kuhakikisha sekta hii inakua bora zaidi ili kupata Taifa lenye tija.

Aidha Profesa Elisante amesisitiza umuhimu wa wazazi kushirikiana kwa karibu na walimu ili kuhakikisha wanafunzi wanapata Elimu iliyo bora ikiwema maadili mema.

“Ndugu zangu tunawenza kabisa tukajenga Taifa lenye watu waadilifu kama tutashirikiana baaina ya walimu na wazazi katika kuhakikisha watoto wetu wanapata Elimu iliyo bora, hapana shaka kabisa msingi wa maadili mema huku ndiko unakoanzia” Alisema Profesa Elisante.

Profesa Elisante aliongeza kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa ,walezi,walimu na jamii kwa ujumla kujenga utamaduni wa kuwafundisha watoto maadili mema, kwani hiyo itawasidia kufikia malengo waliyokusudia.

Profesa Gabriel aliongeza kuwa, ili kuwepo na elimu bora kuna mambo makuu  ya kuzingatia kama uongozi wa shule mzuri wenye mshikamano,wazazi au walezi kutimiza wajibu wao wa kazi na wanafunzi pia kusoma kwa biidii ili kuwapa moyo wazazi wa kulipa ada  kwa wakati  na walimu kufanya jitihada ya kufundisha.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shule hiyo Bibi. Mary Shirima alisema kuwa Shule hiyo ilianzanisha kwa lengo la kusaidia huduma za jammi ambapo Elimu ni moja kati ya huduma hizo.
Bibi. Shirima aliongeza kuwa wao kama wananchi wa kawaidi wanatambua wajibu wa kusaidia jitihada  katika kukuza maendeleo ya nchi ikiwa ni kuonesha kwa vitendo dhana ya ushirikiana baina ya Serikali na Taasisi binafsi.

“Tulianzisha Sunrise kwa utashi na dhana ya kutimiza wajibu wa kusaidia jamii kama mwananchi anayeipenda nchi yake na wajibu wetu kama walezi, walimu na wafanyakazi wote wa shule yetu kuhakikisha watoto wanaohitimu darasa la saba wanafikia malengo yao ya baadae  kwa kushirikiana na wazazi wao”.Alisema Bibi Shirima.

Aidha  Bibi. Shirima alisema kuwa imekuwa ni faraja kwake kuona Serikali inatambua mchango wa wadau wanaojitolea kuwekeza katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu na kuelezea furaha yake kwa kiongozi wa ngazi ya juu wa Serikali kukubali kuwa mgeni rasmi katika mahafali ya Darasa la Saba ambapo  Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo alikubali kuwa mgeni rasmi katika mahali hayo nakuwakilishwa vyema na Naibu Kaitbu Mkuu wa Wizara hiyo.

Shule ya Msingi na Awali Sunrise ilianzishwa mnamo mwaka 1999 ambapo hadi sasa inashereheke mahafali ya Saba kwa wahitimu wa Darasa la Saba ambapo jumla ya wahitimu wa mwka huu ni 66 kati yao Wasichana 42 na Wavulana 

No comments:

Post a Comment

Pages