HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 27, 2014

ANGELS MOMENT WAINGIA JIJINI MWANZA TAYARI KWA MAANDALIZI YA KAMPENI YA MWANAMKE NA UCHUMI, KUWAELIMISHA ZAIDI YA WANAWAKE WAJASIRIAMALI 600 KUTOKA WILAYA ZA MAGU, ILEMELA, NYAMAGANA NA MISUNGWI

Afisa Uhusiano wa TBS, Roida Andusamile pamoja na Meneja wa Kanda ya ziwa wa PPF Bwana Meshach Bandawe wakifuatilia mkutano na waandishi wa habari uliofanyika mapema leo katika ukumbi wa Gold Crest kuwahabarisha kuhusu kampeni ya Mwanamke ya Uchumi itakayofanyika jijini Mwanza tarehe
4-5 Septemba, 2014 katika viwanja vya Mwaloni Kirumba Jijini Mwanza. 
(Na Mpiga Picha Wetu)
 Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Angels Moment, Naima Malima akizungumza na na waandishi wa habari kuhusu Kampeni ya Mwanamke na Akiba inayotarajiwa kufanyika Mkoani Mwanza kuanzia Septemba 4-5, ambapo zaidi ya wanawake wajasiriamali 600 wanatarajiwa kufaidika na mafunzo hayo. 
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Angels Moment, Naima Malima akizungumza na na waandishi wa habari kuhusu Kampeni ya Mwanamke na Akiba inayotarajiwa kufanyika Mkoani Mwanza kuanzia Septemba 4-5, ambapo zaidi ya wanawake wajasiriamali 600 wanatarajiwa kufaidika na mafunzo hayo. 
Afisa Uhusiano wa TBS, Roida Andusamile akielezea jukumu la TBS katika kuwaelimisha wanawake wajasiriamali wa Kitanzania watakaoshiriki katika kampeni ya Mwanamke na Uchumi juu ya ubora na viwango katika bidhaa wanazoandaa.
Afisa Uhusiano wa TBS, Roida Andusamile akielezea jukumu la TBS katika kuwaelimisha wanawake wajasiriamali wa Kitanzania watakaoshiriki katika kampeni ya Mwanamke na Uchumi juu ya ubora na viwango katika bidhaa wanazoandaa.
Meneja wa NSSF Mkoa wa Mwanza, Hamis Fakii akielezea umuhimu wa akinamama kujiwekea akiba katika Mifuko ya Pensheni kwa Maisha yao ya sasa na ya baadae, Pia kujiunga na skimu ya SHIB ili wapate matibabu na familia zao kwa kuchangia pesa kidogo sana.
Afisa Huduma na Elimu wa TRA Mkoa wa Mwanza, utufyo Mtafya ambae ni  akielezea umuhimu wa wanawake wajasiriamali wa kitanzania kutunza mahesabu yao kwa kutumia mashine za EFD.
Meneja wa Kanda ya Ziwa wa PPF, Meshach Bandawe akielezea kwa wanahabari jinsi PPF inavyosaidia wanawake wajasiriamali walio katika sekta isiyo rasmi kwa kuwapa mikopo kupitia SACCOS.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Angels Moment, Naima Malima akizungumza na na waandishi wa habari kuhusu Kampeni ya Mwanamke na Akiba inayotarajiwa kufanyika Mkoani Mwanza kuanzia Septemba 4-5, ambapo zaidi ya wanawake wajasiriamali 600 wanatarajiwa kufaidika na mafunzo hayo.

Na Mwandishi Wetu
ZAIDI  ya wanawake 600 mkoani Mwanza, wanatalajia kupata elimu juu ya ujasiriamali , Usimamizi wa fedha, uwekaji akiba pamoja na mafunzo ya afya bora.

Akina mama na vijana kutoka katika  wilaya za Magu, Ilemela, Misungwi na Nyamagana  watashiliki  kikamilifu katika kampeni hii itakayotolewa na taasisi ya ANGELS MOMENTS ya jijini Dar es salaam.

 Akizungumza  wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Mwanza jana,Mkurugenzi wa Taasisi ya ANGELS MOMENTS Naima Malima,  alisema  kampeni hii inalenga kuwajengea uwezo na ujuzi wa kusimamia fedha zao kwa lengo la kunyanyua uwezo wao wa kiuchumi pamoja na familia zao.

Naima alisema kampeni hiyo imeanzia mkoani Mwanza kwa kutambua fursa zilizopo mkoani hapo, hivyo wanawake wa mkoa huo watapewa elimu ya msingi ya kibiashara na kuchochea na mna ya kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo ndani na nje ya mkoa wa Mwanza.

“Kwa kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii pamoja na taasisi ya WAMA tunatarajia kuwafikia wanawake wa vikundi vyote vya kijamii, SACCOS, AMCOS, VICOBA na makundi mengine ya kijamii yanayojihusisha na wajasiriamali na hivyo kampeni hii itawawezesha kujiongezea uwezo wa kupata wateja wa bidhaa na huduma zao na kujitangaza zaidi”. alisema Naima.

Aidha alisema pamoja na mkoa wa Mwanza kampeni ya Mwanamke na Uchumi pia itafanyika katika mikoa ya Tanga, Kigoma, Dodoma, Pwani, Ruvuma na Lindi kuanzia mwishoni na mwanzoni mwa miezi ya septemba hadi Januari 2015 mtawalia.

Alimalizia kwa kuwaomba wanawake na vijana wote wa mkowa wa Mwanza kufika bila kukosa Septemba 4 na 5 katika viwanja vya Mwaloni, Kirumba jijini Mwanza.

No comments:

Post a Comment

Pages