HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 26, 2014

MKAZI WA KOROGWE ADAI FIDIA YA SHAMBA


MKAZI wa Kata ya Kilole wilayani Korogwe Tanga, Anna Tindwa (54),  amemuomba Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuingilia kati kitendo cha Halmashauri ya wailaya hiyo kuchelewesha kumlipa fidia ya shamba lake kwa zidi ya miaka tisa.

Fidia anayodai imetokana na Serikali ya Mtaa wa Kwamngumi katika kata hiyo kulichukua shamba lake mwaka 2006 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kata Kilole.

Akizungumza katika jijini Dar es Salaam, Anna, alisema hadi sasa hajui kuna sababu gani inayofanya asilipwe fidia hiyo wakati wenzake wanne wamekwishalipwa.

Alisema, amefikia hatua hiyo ya kumtaka waziri amsaidie, kwasababu tangu imefanyika tathimini ya kwanza ya mazao ikiwa ni pamoja na nyumba yake ni muda mrefu hata hivyo haelezwi sababu inayochelewesha fidia hiyo,hadi leo hajui atalipwa shilingi ngapi.

Anna, alitaja mazao ambayo yalikuwemo katika shamba hilo kuwa ni minazi, miembe, michungwa na nyumba ambapo hivi sasa mali hizo zote zinaharibika.

Alisema, kuharibika kwa mali hizo kunatokana na serikali kumzuia kufanya shughuli zozote za maendeleo katika shamba hilo tangu mwaka 2006.

“Kinacho nisikitisha kunahatari nikazulumiwa mali zangu kwa sababu hivi sasa baadhi ya mazao yamekwisha haribiwa kwa mfano miembe, michungwa na mifenesi imekatwa wakati hatujalipwa haki yetu.

“Kwa kuthibitisha hilo angalia baada ya kutufanyia tathimini ya kwanza ambayo ilikuwa sahihi sasa wamekuja kufanya nyingine ambayo kuna baadhi ya mazao yameishaharibiwa hivyo kupunguza thamani ya fidia, hii siikubali nataka itumike ile ile ya kwanza,”alisema Anna.

Anna, alisema yeye ni mjane ambaye hana mtu wa kumsaidia kutokana na mazingira hayo alitegemea angelipwa fidia hiyo mapema ili ikamsadie katika ujenzi wa makazi mapya.

“Naomba nilipwe fidia kwani ni haki yangu inanisikitisha, ni muda mrefu nimekuwa nikifuatilia fidia ya malipo bila mafanikio kwani napigwa danadana katika kila ofisi za halmashauri ya korogwe sasa ndio maana nimeamua kumuandukia barua waziri Profesa Anna Tibaijuka,”alilalamika Anna.

Aliongeza kwa kusema kuwa anamuomba waziri huyo amsaidie katika ulipwaji wa fidia hiyo, ili iweze kumsaidia katika ujenzi wa nyumba yake ambayo paa lake limeezuliwa na upepo.

Alipotafutwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhusu ucheleweshaji huo, Lewis Kalinjuna:Tatizo hilo nimelisikia sikia, lakini nitalifuatilia vizuri ili ni mjue huyo mama niweze kumsaidia.
Kuhusu ucheleweshaji wa ulipaji fidia hiyo kwa muda wa miaka nane, Mkurugenzi huyo, alisema haoni kama kuna ucheleweshaji wowote bali alimtaka Anna aendelee kusubiri.

No comments:

Post a Comment

Pages