HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 14, 2014

SIRI YA KUWAFUKUZA WAKAZI WANAOISHI KATIKA MSITU WA KAZIMZUMBWI YABAINIKA

SIRI ya mgogoro wa kutaka kuwafukuzwa wakazi wa vijiji vya Chanika wilayani Ilala jijini Dar es Salaa kwa madai kuwa wamevamia msitu wa Kazimzumbwi yabainika.

Hayo yaliyasemwa na Mjumbe wa Kamati ya wakazi na wakulima wa vijiji hivyo, Hamza Khamisi, alipozungumza kuhusu propaganda hizo zinazosambazwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, tangu mwaka 1992.

Alisema, siri ya kufukuzwa wakazi hao inatokana serikali kuingia makubaliano na kampuni moja ya kigeni (jina tunalo), kutoka nchini Norway hivi karibuni kwa ajili ya kuanzisha mradi ambao haujawekwa wazi.

“Kihistoria na kisayansi eneo la Chanika na vijiji vyake vya Nzasa, Kimwani na Nyeburu sisehemu hata kidogo ya msitu wa hifadhi ya Kazimzumbwi,”alisema Khamisi.

Alisema ikumbukwe kuwa baada ya makubaliano hayo ndipo wizara ya Maliasili na Utalii ilipoamua kimabavu kuanzisha mgogoro huo, bila ya kufuata utaratibu wa kisheria, kupanua mipaka yake kinyume na ule wa asili wa mwaka 1954.

“Kamati yetu ywa wakulima imekuwa ikishawishiwa kwa fedha ili ikubali kuwashauri kuwashauri wenzetu tukubali kuondoka kwamba tutalipwa vizuri jambo linalotupa wasiwasi.

“Ndugu mwandishi tunayo CD ya mkutano kati yetu na viongozi wa ngazi ya juu, uliyofanyika Kibaha, viongozi wakidai kupoteza mradi huo wa wazungu nchi itapoteza fedha nyingi jambo ambalo itakuwa aibu kwa nchi.

“Ninachoeleza wala sio madai tumefanya vikao viwili vinavyowahusu hao wazungu cha kwanza ilikuwa Buguruni na hcho cha mkoani pwani viongozi waliokuwepo watakapoona hii taarifa hawataweza kubisha,”alidai Khamisi.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza, likakaririwa na vyombo vya habari akisema serikali ya mkoa wake imeshapokea maelekezo ya serikali na itatekeleza agizo hilo ambalo litasaidia kuirejesha misitu hiyo katika hali yake ya kawaida.

Alisema uharibifu huo umelitia aibu taifa mbele ya jumuiya ya kimataifa ambayo inatambua umuhimu wa misitu ya Kazimzumbwi kimazingira na kuboresha hali ya hewa ya jiji la Dar es Salaam.

Mwanzoni mwa Desemba mwaka huu  jijini katika mkutano wa kitaifa wa msitu huo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Razalo Nyalandu, alisema kamwe serikali haiwezi kuendelea kuwavumilia wavamizi hao ambao wamesababisha uharibifu mkubwa wa mazingira ya misitu hiyo ya Kazimzumbwi iliyohifadhiwa kisheria tangu mwaka 1954 na

Nyalandu aliongeza kuwa katika operesheni hiyo kubwa itakayofanyika baadae mwezi huu serikaili haitatambua hati au vibali vya watu wanaoishi katika misitu hiyo kwani wanaishi humo kinyume cha sheria na ametaka watu wote humo kuanza kuondoka kwa hiari kabla ya muda huo na amebadilisha hati zote zinazotumiwa na wavamizi hao.

No comments:

Post a Comment

Pages