HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 18, 2014

TTCL YAZINDUA PROMOSHENI MPYA

Meneja Bidhaa za Intanet wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Abdul Mombokaleo akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa promosheni mpya inayotoa fursa kwa mteja kufurahia huduma ya intaneti na kujipatia modem ya bure. Kulia ni Mkuu wa Huduma kwa Wateja, Laibu Leonard. (Picha na Francis Dande)
Meneja Bidhaa za Intanet wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Abdul Mombokaleoakionyesha vipeperushi vyenye maelekezo kuhusu promosheni hiyo. Kulia ni Mkuu wa Huduma kwa Wateja, Laibu Leonard na Ofisa Uhusiano wa TTCL, Edwin Mashaki.

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL), imezindua promosheni mpya inayotoa fursa kwa mteja kufurahia huduma ya intaneti na kujipatia modem ya bure.

Hayo yalisemwa na Meneja wa wa Bidhaa za Intaneti, Abdul Mambokaleo, wakati alipozungumza na wandishi wa habari kuhusu promosheni hiyo, jijini Dar es Salaam.

“Promosheni hii, ya ‘Dili la Ukweli’ ni muendelezo wa kampuni yetu katika kuwapatia wateja wetu kile wanachokihitaji wapatiwe,”alisema Mambokaleo.

Alisema, promosheni hiyo inatoa fursa kwa wateja kufurahia modem ya bure pamoja na vifurushi ambavyo vimepunguzwa bei kwa kiwango ambacho kitamfanya Mtanzania wa kawaida aweze kutumia humuduma hiyo.

“Kupata modem ya bure mteja atapaswa kununua intaneti bila kikomo kw ash 20,000 ambayo itatumika ndani ya mwezi mzima.

“Huduma hii ni kwa wateja wapya tu, kwa mteja mwenye modem tumempa fursa ya kuchagua vifurushi ambavyo vimepunguzwa bei,”alisema Mambokaleo. 


Mambokaleo alisema promosheni hiyo ya Dili la Ukweli inatoa fursa kwa mteja kufurahia punguzo la bei ya vifurushi vya intaneti vya siku, wiki na mwezi kwa bei nafuu, kwa taarifa zaidi kila mteja anaweza kutembelea ofisi zao.

No comments:

Post a Comment

Pages