Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Amani, Alex Msama akifafanua jambo
wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu
waimbaji watakaotumbuiza katika tamasha hilo litakalofanyika Oktoba 4 kwenye
uwanja wa taifa. Kushoto ni Mratibu wa tamasha hilo, Benno John Chelele.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Amani, Alex Msama akifafanua jambo
wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu
waimbaji watakaotumbuiza katika tamasha hilo litakalofanyika Oktoba 4 kwenye
uwanja wa taifa. Kushoto ni Mratibu wa tamasha hilo, Benno John Chelele.
Na Mwandishi Wetu
Na Mwandishi Wetu
MALKIA
wa muziki wa Injili nchini na Afrika Mashariki na Kati, Rose Muhando, amethibitishwa
kushiriki tamasha maalum la Kuombea Amani Uchaguzi Mkuu litakalofanyika Oktoba
4, jijini Dar es Salaam.
Muhando,
anakuwa mwimbaji wa nne kutajwa katika orodha ya watakaopamba tukio hilo linalobeba umuhimu
wa aina yake katika kuhimiza na kusisitiza amani na utulivu wakati na baada ya
uchaguzi mkuu wenye ushindani mkubwa.
Mwanadada
huyo mwenye sauti, uwezo na vipaji vya aina yake katika huduma hiyo ya uimbaji,
anaungana na wakali wengine kama Bonny
Mwaitege, Christopher Mwahangila na Upendo Nkone.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam leo, Alex Msama ambaye ni Mwenyekiti
wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha hilo
litakalofanyika mikoa 10 nchini, alisema Rose tayari amethibitisha.
"Maaandalizi
ya Tamasha la kuombea amani ya nchi yetu ambayo ni tunu ya aina yake tuliyojaaliwa
na Mwenyezi Mungu, yanakwenda vizuri kwani
Rose naye ataungana na wengine siku hiyo,” alisema Msama.
Msama
alisema Tamasha hilo
linalolenga kuwaleta pamoja watanzania bila kujali tofauti zao za dini, kabila,
itikadi wala rika, litahudhuriwa pia na viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwamo
wale wa kiroho kwa ajili ya kuombea amani uchaguzi mkuu.
Alisema
wakiwa waratibu wa matamasha ya muziki wa injili kwa miaka mingi sasa, wameona
ni jambo jema kuwaleta pamoja watu kuomba Mungu uchaguzi mkuu uwe wa amani na
utulivu.
Msama
alisema hilo ni
jambo muhimu kwa kuzingatia baadhi ya mitafaruku ya kisiasa imekuwa ikianzia katika
harakati za uchaguzi, hivyo ni suala la busara kumwomba Mungu autangulie
uchaguzi huo na watu wake.
Alisema
siku hiyo maelfu yatakayojitokeza wakiongozwa na watumishi wa Mungu,
wataukabidhi mikononi mwa Mungu uchaguzi huo ili uweze kufanyika kwa amani na
utulivu bila kuacha makovu na athari kwa wananchi.
Msama
alisema, mbali ya kuuombea uchaguzi mkuu, Tamasha hilo pia litatumika kumuaga rasmi Rais wa
Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete ambaye amekuwa mdau mkubwa wa muziki wa injili
nchini.
No comments:
Post a Comment