HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 24, 2016

Mashindano ya Ubingwa wa Mchezo wa Chess Afrika Kanda ya 4.2 yaanza jijini Dar es Salaam

Mwenyekiti wa Mfuko wa mchezo wa Chess Tanzania (TCF) Bw. Vinay Choudary akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa Mashindano ya Ubingwa wa Afrika, Kanda ya 4.2 ya mchezo huo jana jijini Dar es Salaam. Kanda ya 4.2 inahusisha nTimu kutoka nchi za Misri, Ethiopia, Eritria, Sudan, Sudani Kusini, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia,Djibouti na wenyeji Tanzania.Mashindano hayo yameanza jana tarehe 23 April hadi April 31ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye.
  Mwenyekiti wa Chama cha Mchezo wa Chess Tanzania (TCA) Bw. Geofrey Mwanyika akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa Mashindano ya Ubingwa wa Afrika, Kanda ya 4.2 ya Mchezo huo jana jijini Dar es Salaam. Kanda ya 4.2 inahusisha Timu kutoka nchi za Misri, Ethiopia, Eritria, Sudan, Sudani Kusini, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia,Djibouti na wenyeji Tanzania.
Rais wa Chama cha Mchezo wa Chess Malawi, ambaye pia ni ni Mbunge mstaafu wa wa Bunge La nchi hiyo Mhe. Kezzie Msukwa akizungumza namna Mhcezo huo Mchezo huo ulivyopiga hatua nchini Tanzania ukilinganisha na kwao jana jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa Mashindano ya Ubingwa wa Afrika, Kanda ya 4.2 ya Mchezo huo jana jijini Dar es Salaam. Kanda ya 4.2 inahusisha Timu kutoka nchi za Misri, Ethiopia, Eritria, Sudan, Sudani Kusini, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia,Djibouti na wenyeji Tanzania. Mbunge huyo wa zamani wa Malawi yupo nchini kama Mwamuzi katika mashindano hayo.
 Baadhi ya washiriki wa Mashindano ya Ubingwa wa Chess Afrika, Kanda ya 4.2 kimchezo huo wakiendelea kuchuana jana jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yanendelea katika Ukumbu uliopo Hotel ya Peackok ambapo mshindi katika mashindano hayo atajinyakulia kitika cha Euro 3000. Picha na: Frank Shija,WHUSM

No comments:

Post a Comment

Pages