HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 08, 2016

MFUMUKO WA BEI WAPUNGUA KW ASILIMIA 5.4

NA NEEMA MWAMPAMBA

MFUMUKO wa bei wa Taifa kwa mwezi machi 2016 umepungua hadi asilimia 5.4 kutoka asilimia 5.6 ya februari 2016.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS), Albina Chuwa, alisema hali hii inamaanisha kuwa kasi ya upandaji bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi machi,2016 imepungua ukilinganisha na mwaka ulioishia februari 2016.

Alisema Fahirisi za bei zimeongezeka hadi 101.93 kwa mwezi machi 2016 kutoka 96.69 mwezi machi 2015 huku mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi machi 2016 umepungua hadi 8.3 kutoka asilimia 9.5 ilivyokuwa mwezi februari 2016.

Alisema kupungua kwa mfumo wa bei wa mwezi machi kumechangiwa hasa na kupungua kwa bei za bidhaa zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoisha mwezi machi 2016 zikilinganishwa  na bei za mwezi machi 2015.

“pamoja na kupungua kwa kasi ya upandaji wa bei za bidhaa kwa mwaka ulioishia mwezi machi 2016, kuna baadhi ya bidhaa zilizoonesha kuongezeka katika kipindi hicho zikiwa ni pamoja na bei za mchele kwa asilimia 21.7, mahindi 47.8 na vyakula kwenye migahawa 16.2”alisema Chuwa.

Akizungumzia thamani ya shilingi ya Tanzania kwa mwezi machi Chuwa alisema Sh.100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma umefikia shilingi 98 na sent 11 mwezi machi mwaka huu kutoka mwezi Desemb mwaka jana ikilinganishwa na shilingi  98 na senti 58 ya  februari mwaka huu.

Pia alisema mfumuko wa bei nchini una mwelekeo unaofanana na baadhi ya nchi nyingine za Afrika Mashariki ambapo mfumuko wa bei kwa mwezi machi nchini Kenya umepungua hadi asilimia 6.45 kutoka asilimia 6.84 mwezi februari 2016 na Uganda imefika 6.2 kutoka 7.0.

No comments:

Post a Comment

Pages