HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 21, 2017

Kongamano la Usafiri wa Anga

 Wabunge wa zamani wa majimbo ya Nachingwea na Lilundi, Mhe. Maokola Majogo (kulia) na Anna Abdallah wakipata maelezo mbalimbali ya Kiwanja cha Ndege cha Mtwara, kutoka kwa Mhandisi Kedrick Chawe na Bi. Harieth Nyalusi katika maonesho yanayokwenda sambamba na Kongamano la Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga, lililomalizika leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam.
 Bw. Geoffrey Tupper (kulia) akikusanya makabrasha mbalimbali yanayotoa maelezo ya viwanja vya ndege kutoka katika meza ya maonesho ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), yaliyokuwa yakienda sambamba na Kongamano  Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga, lililomalizika leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Bi. Fatma Matimba na Mhandisi Kedrick Chawe wa TAA.
 Mhandisi Kedrick Chawe akimfafanulia masuala mbalimbali ya Viwanja vya ndege, Bi. Mwamini Mohamed aliyetaka kujua ujenzi wa jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII), wakati wa Kongamano la Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga lililomalizika leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
 Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Johannes Munanka akichangia mada kwenye Kongamano la siku mbili la Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga, lililomalizika leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
 Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) (wa tatu kutoka kushoto), Bw. Salim Msangi akihudumia wananchi waliofika kutaka maelezo mbalimbali kwenye meza ya maonesho ya TAA yaliyokwenda sambamba na Kongamano la Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga lililomalizika leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam. Wengine kuanzia kulia ni Mhandisi Kedrick Chawe, Bi. Harieth Nyalusi na Bi. Rose Comino wa TAA.

No comments:

Post a Comment

Pages