HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 15, 2017

Tufanye Mazoezi Kumuenzi Mwalimu Nyerere

Wananchi wa Mkoa wa Rukwa wameshauriwa kuweka utamaduni wa kugfanya mazoezi kila siku kwa lengo la kuyaenzi Maisha ya Hayati Baba wa Taifa, kwani kufanya hivyo ni kwa faida ya afya zetu  wenyewe.

Yamesemwa hayo na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen katika kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere katika kiwanja wa Nelson Mandela, mjini Sumbawanga.

Maadhimisho hayo yaliyokwenda sambamba na jumamosi ya pili ya mazoezi pamoja na kilele cha wiki ya vijana wananchi walijitokeza kwa wingi asubuhi kwaajili ya kushiriki kwenye mbio zilizoanza ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na kuelekea kwenye jkiwanja hicho cha mpira kikubwa mkoani Rukwa.

Amesema kuwa watanzania wameacha kufanya mazoezi hali inayopelekea kunyemelewa na magonjwa mbalimbali hali inayopelekea kupunguza nguvu kazi ya taifa.

Ameongeza kuwa Katika kuiweka afya yake vizuri, hutumia dakika 20 asubuhi kufanya mazoezi kabla ya kuelekea ofisini hali iliyopelekea kuoneka na afya nzuri mbali na kuwa na umri mkubwa.

“Msinione bado nipo fiti ni kwasababu ya kufanya mazoezi kila siku kwa dakika 20 kabla sijaingia ofisini, mazoezi haya ni faida yetu wenyewewe, sio faida ya Rais, Makamu wa Rais wala Waziri Mkuu, na Katika kuona kuwa watanzania wameacha mazoezi Serikali ya ikaagiza kila jumamosi ya pili ya mwezi iwe ya mazoezi si kwasababu nyingine bali ni kuendelea kutunza afya zetu,” Alifafanua.

Pia alitumia nafasi hiyo kumuagiza Katibu Tawala wa Mkoawa Rukwa kuhakikisha kuwa anaweka utaratibu wa kuhakikisha kila mtumishi wa serikali anashiriki kwenye mazoezi hayo ili kuimarisha afya zao na kuendeleza kulijenga taifa.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bernard Makali katika kuisemea kilelel cha wiki ya vijana, amewataka vijana wote mkoani humo kuandika maoni juu ya fani watakazotaka zifundishwe katika chuo kipya cha ufundi VETA kinachotarajiwa kuanza kujengwa katika makao makuu ya Mkoa huoMjini Sumbawanga.

“Katika kuhakikisha huduma mbalimbali za kiufundi zinapatika katika Mkoa wetu, hivi karibuni serikali itaanza kujenga chuoi cha ufundi VETA cha kisasa kabisa, hivyo make tayari kwa hilo na wamekuja kutaka kutaka maoni juu ya fani ambazo tunataka zifundishwe kwenye chuo hivyo ni fursa yenbu kuleta maoni ya fani mnazotaka zifundiswe kwenye chuo hicho,” Alimalizia.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Kamishna Mstaafu Zelote Stephen (kulia), akipimwa macho zoezi lililoendeshwa kwa wananchi wote waliohudhuria katika maadhimisho ya kifo baba wa Taifa, Kiwanja cha Mandela, Mjini Sumbawanga, baadaya kupima alionekana hana tatizo.

No comments:

Post a Comment

Pages