HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 27, 2018

Airtel yatangaza washindi wa promosheni ya AMSHA AMSHA na Airtel Money na ushinde


Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Jackson Mmbando, akizungumza waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza washindi wa promosheni ya 'Amsha Amsha Ushinde na Airtel Money' kwa kushirikiana na Sportpesa. Kulia ni Meneja Uhusiano Sabrina Msuya na Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahati, Ahmed Hemed. (Na Mpiga Picha Wetu).

Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Jackson Mmbando, akionyesha moja ya zawadi walizopata washindi wa Amsha Amsha Ushinde na Airtel Money kwa kushirikiana na Sportpesa, Dar es Salaam jana. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Sportpesa, Sabrina Msuya na Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahati, Ahmed Hemed.
Meneja Uhusiano wa Sportpesa, Sabrina Msuya, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa hafla ya kutangaza washindi wa Amsha Amsha Ushinde na Airtel Money.

Na Mwandishi Wetu

 Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na SportPesa imetangaza washindi wa kwanza wa promosheni ya mwezi mmoja ya AMSHA AMSHA na Airtel Money na ushinde ambayo ilizinduliwa Juni 14 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kutangaza washindi hao, Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando alisema kuwa droo ya kupata washindi hao imesimamiwa na kuchezesha kwa wazi na Bodi ya Michezo ya kubahatisha Tanzania ambayo ndio wenye jukumu la kusimamia michezo yote ya bahati nasibu hapa nchini.

Kama mlivyoona hapa kwa siku ya leo, droo yetu imechezesha kwa uwazi na hii inaamanisha kila mteja anayo fursa ya kuwa mshindi alisema Mmbando huku akiongeza kuwa kile mteja wa Airtel Money anachotakiwa kukifanya ni kuhakikisha anabet siku ambayo droo iko wazi na moja kwa moja namba yake itaingizwa kwenye droo ya wiki. ‘Mteja atatakiwa kubet siku ya droo ili kupata nafasi ya kuwa moja ya washindi, alisema Nchuda huku akiongeza kuwa wateja wanatakiwa kuhahakikisha kuwa wanayo pesa kwenye akaunti yao ya SportPesa.

Mmbando alisema kuwa washindi wa leo kumi wamejishindia simu mpya za smartphone kila mmoja, wengine kumi wamejishindia jezi za timu za Simba na Yanga huku wengine kumi kila mmoja akijishindia tiketi ya kushuhudia mechi za Simba na Yanga kwa msimu wote wa 2018/2019. Natoa rai kwa wateja wote wa Airtel kushiriki kwenye hii promosheni ya AMSHA AMSHA USHINDE NA AIRTEL MONEY kwani muda bado hupo na zawadi kwa washindi bado ni nyingi, alisema Nchunda huku akiongeza kuwa mshindi mmoja kwa siku ya leo amejishindia TV mpya yenye inchi 32 pamoja na ving’amuzi kutoka Star Times.

AMSHA AMSHA USHINDE NA AIRTEL MONEY inatoa nafasi kwa wateja wetu wa Airtel Money kuweza kujishindia zawadi kabambe kwa kubet kwa kutumia Airtel Money. ‘Airtel siku zote tunaleta huduma na bidhaa zenye ubunifu na za kutuweka karibu na wateja wetu. Tunaelewa ya kwamba michezo pamoja na mambo ya kubet imekuwa na maisha ya kawaida kwa wateja wetu. Kwa kuzindua promosheni hii ambayo tumeshirikiana na SportPesa inatoa nafasi nyingine ya kuendelea kutuweka karibu na wateja wetu’, aliongeza Mmbando.

Kwa upande wake, Meneja Uhusiani wa SportPesa Sabrina Msuya alisema kuwa tangu kuzinduliwa kwa promosheni ya AMSHA AMSHA USHINDE NA AIRTEL MONEY 14 Juni mwaka huu, droo imekuwa wazi kila siku kuanzia saa sita usiku mpaka 11:59 kwa siku inayofuata kwa muda wote wa promosheni na kila mteja anachotakiwa kufanya ni kubet siku ya droo na namba yake itaingizwa kwenye droo moja kwa moja.

Bi Sabrina alisema zawadi za kila siku ni simu mpya za smartphone, jezi za Simba na Yanga pamoja na tiketi za kushuhudia mechi za Simba na Yanga msimu wote huu huku za kila wiki ikiwa na TV mpya yenye inchi 32 pamoja na ving’amuzi kutoka Star Times.
 
Kile ambacho mteja anachotakiwa kufanya ni kujiandikisha, kuweka pesa kwenye akaunti yake ya SportPesa kwa kutumia Airtel Money halafu ndio abeti, alisema Abbas huku akiongeza kuwa washindi wanaweza kuchukua zawadi zao kutoka duka lolote la Airtel hapa nchini.

No comments:

Post a Comment

Pages