HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 15, 2019

NATIONAL CROSS COUNTRY 2019 HELD IN MOSHI


MASHINDANO ya Taifa ya Wazi ya Mbio za Nyika ‘National Open Cross Country 2019’ yanatarajiwa kufanyika kwenye viwanja vya Gofu mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, Februari 16 mwaka huu.

Kwa majibu wa Katibu Msaidizi wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Ombeni Zavalla, mashindano hayo yatakuwa maalum kuchagua timu ya Taifa itakayoiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Nyika ya Dunia na mwanariadha yeyote anaruhusiwa kushiriki.

Msimu wa 43 wa Mashindano ya Nyika ya Dunia unatarajiwa kufanyika Aarhus, nchini Denmark, Machi 30 mwaka huu.
Zavalla, alisema mikoa yote imeishatàarifiwa rasmi kuhusu mashindano hayo na wanariadha watakaofanya vizuri watachaguliwa timu ya Taifa.

Alisema mashindano hayo yatakuwa kwa upande wa Wanawake Sr, Wanaume Sr, Wavulana Jr na Wasichana Jr.

Katibu huyo Msaidizi, aliongeza baada ya mashindano hayo ya Taifa ya Nyika kumalizika, Kamati ya Ufundi itachagua makocha watakaoingia kambini na timu itakayokuwa imechaguliwa mara moja huko Mbulu mkoani Manyara kujiachia na mashindano hayo ya Dunia.

Mbio za Nyika za Dunia zilizopita zilifanyika barani Afrika, Kampala nchini Uganda, 2017.

No comments:

Post a Comment

Pages