HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 31, 2019

SIMBA KUIKABILI MBAO FC LEO

NA JOHN MARWA
WANATOKAJE! ndivyo unaweza kusema kuelekea mchezo wa leo mjini Morogoro Mabingwa watetezi wa  Ligi Kuu Tanzania Bara TPL Simba SC wakiwakabili vilivyo wabishi wa jijini Mwanza, Mbao FC.
Simba wanashuka kwenye mtanange huo wakiwa na hasira za kulipa kisasi cha kuchapika bao 1-0 pambano la ungwe ya kwanza lililopigwa Septemba 20, 2018 Uwanja wa Kirumba jijini Mwanza.
Wakitoka kupata mafanikio makubwa katika Ligi ya Mabingwa Afrika CAF CL na kuwasasambua Ruvu Shooting mabao 2-0, wanaingia fulu mzuka kuwakabili Mbao ambao wamewatia doa msimu huu ikiwa timu pekee ilkiyoifunga Simba hadi sasa.
Simba wanahitaji ushindi kuendeleza mapambano ya kutetea ubingwa wao, wakiwa wameshacheza michezo 21 pointi 54 nafasi ya tatu mechi 7 nyuma ya vinara wa TPL Yanga wenye pointi 67 mechi 28.
Wabishi wa Mbao wanashuka kwenye mtanange wa leo wakishika nafasi ya 15 kwenye msimamo na pointi 36 za michezo 30.
Mbao FC wamefanikiwa kushinda mechi tisa sare tisa huku wakipoteza 12, wamefunga mabao 19 na kuruhusu 29, wastani wa kufumania nyavu ni 0.63 katika kila mchezo na wa kufungwa ni 0.96, sawa na bao moja kila mechi.
Wakati huo kikosi cha Mbelgiji Patrick Aussems badaa ya kushuka dimbani mara 21, kimeshinda mapambano 17 sare tatu na kupoteza dhidi ya wabishi hao.
Hadi sasa Simba wametikisa nyavu za wapinzani wao mara 45, huku wakiwa wameruhusu mabao machache zaidi hadi sasa yakiwa  ni saba ya kufungwa.
Takwimu zinaonyesha Simba kuwa na safu imara zaidi sambamba na safu ya ushambuliaji ikiwa imetupia mabao hayo 45 michezo michache zaidi ya wapinzania wake wa karibu Yanga na Azam wakiwa na mabao 46 ya kufunga ndani ya michezo 28.
Wastani wa Simba kutikisa nyavu katika kila mchezo ni mabao 2.14 huku wakiruhusu lango lao kutikiswa ni 0.33 kwa mtanange.
Katika michezo mitano iliyopita kunako TPL Simba wamepata matokeo kwa asilimia 100, wakishinda michoze yote  huku Mbao ni asilimia 80, wakishinda mmoja na kupoteza minne.
Katika michezo 15 waliyocheza ugenini Mbao hadi sasa wameshinda mechi mbili sare tano na kupoteza minane, huku Simba ni michezo 10 wakishinda  nane sare moja na kupoteza moja.
Wakati katika michezo ya nyumbani Mbao wamecheza michezo 15 wakipata matokeo mechi saba, sare nne na kupoteza minne, huku Mnyama akiwa amecheza mechi 11 ya kushinda 9 na sare mbili wakiwa haawajapoteza mchezo.
Kibarua kizito katika mtanange huo kitakuwa kwa Kocha wa Mbao Salum Mayanga ukiwa mchezo wake wa kwanza tangu achukue mikoba ya Ally Bushiri ‘Benitez’ baada ya kuvunjiwa mkataba wake na Klabu hiyo kwa madai ya kutoridhishwa na matokeo waliyopata.
Mayanga anakuwa Kocha wa tatu msimu huu kuinoa timu hiyo huku macho na masikio ya wengi yakimtazama jinsi gani itaingia kuinusuru Mbao kushuka daraja msimu huu.

No comments:

Post a Comment

Pages