HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 17, 2019

Makonda afurahishwa na kasi ya ujenzi Wa Ofisi ya Shule ya Sekondari Kisauke

NA MWANDISHI WETU

MKUU Wa Mkoa Wa Dar Es Salaam, amesema kasi inayoendelea katika ujenzi wa Ofisi ya Waalimu Shule ya Sekondari Kisauke iliyopo Wilaya ya Kinondoni Kata ya Wazo hili. 

Amesema lengo la  ujenzi Wa Ofisi hiyo ya waalimu ni Kuona Waalimu wanaishi katika mazingira mazuri na matumaini yake  mwisho Wa mwezi Wa 5 Ofisi hiyo itakuwa imekamilika. 

"Tumeona tujenge Ofisi hii kwanza kuwapa heshima Waalimu kwani wanavyotumia choo kimoja na Wanafunzi inashusha heshima na inapelekea baadhi ya wanafunzi kupewa kesi za utovu Wa nidhamu hivyo kukamilika huku tunategemea tunakwenda kutengeneza Mazingira rafiki kwa Waalimu wakiwa katika Mazingira mazuri hata matokeo yatapatikana mazuri kwani watakuwa na uwezo Wa kubuni mikakati ya kufaulu kwa wanafunzi" anasema Makonda. 

Aidha Makonda aliongeza na kusema kuwa lengo la  kufanya ziara hiyo ni kukagua miradi ya Maendeleo ili kile  kilichopo kwenye karatasi kiendane uhalisia, ipo  miradi mbali mbali inayotekelezwa ikiwamo miradi ya ujenzi wa Hospitali, vituo vya Afya na Masoko .

No comments:

Post a Comment

Pages