HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 15, 2019

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AZUNGUMZA NA ABIRIA WA KIVUKO KATIKA ENEO LA BUSISI SENGEREMA MKOANI MWANZA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Abiria wa Kivuko cha MV Mwanza na MV Misungwi kuhusu ujenzi wa Daraja  litakalopita ziwani katika eneo la Kigongo na Busisi mkoani Mwanza. Mkandarasi wa Daraja hilo anatarajiwa kupatikana ndani ya miezi miwili na Daraja hilo litakuwa na urefu wa kilometa tatu zitakazopita majini. Daraja hilo litagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 300
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono abiria wa Kivuko cha MV Mwanza na MV Misungwi mara baada ya kuzungumza nao katika eneo la Busisi Sengerema mkoani Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akielekea kupanda Kivuko cha MV Mwanza katika eneo la Busisi wakati akitokea Geita. PICHA NA IKULU.

No comments:

Post a Comment

Pages