HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 31, 2019

SERIKALI KUIWEZESHA SEKTA YA MICHEZO

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, akizungumza na wadau mbalimbali kuhusu michezo mkoani Kagera.


NA LYDIA LUGAKILA, BUKOBA

Serikali ya Tanzania imejipanga  kumaliza changamoto ya miundombinu mibovu ya  viwanja vya mpira nchini ili kuiwezesha sekta ya michezo kufanya vizuri.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, akiwa mkoani Kagera katika mkutano na  wadau wa sekta ya habari utamaduni sanaa na michezo uliofanyika katika ukumbi wa mkoa uliopo Manispaa ya Bukoba .

Waziri Mwakyembe amesema kuwa anatambua sekta ya michezo kuwa  sehemu muhimu na kuwa  wana michezo wanafanya kazi kubwa licha ya kukumbana na  changamoto ya  miundo mbinu  mibovu ya viwanja  vya michezo.

 amesema  kuwa tatizo hili la miundo mbinu mibovu ya viwanja limekuwa likipigiwa kelele mara kwa mara  na wanamichezo licha ya kuonyesha  juhudi kubwa katika michezo kwa kuendana na miundo mbinu hiyo  mibovu.
‘’ changamoto hii itamalizika mwaka huu   tutalifanyia kazi jambo hili ili kupunguze kelele za viwanja vibovu vya soka nchini.

Katika hatua nyingine waziri Mwakyembe amewataka wananchi  mkoani  Kagera  na  Mikoa ya jirani kuwa  septemba  4 mwaka huu.

Licha ya Changamoto hiyo waziri huyo amewasihi wana michezo hao kutokata tamaa huku akiitaka Mikoa ya jirani  na wana kagera kwa ujumla kujitokeza kwa wingi  Septemba  4 mwezi hujao kuishangilia timu ya  taifa stars inakutana kumenyana  na timu ya Burundi  mchezo ambao ameuataja kuwa ni  muhimu sana kwa watanzania utakaifanya timu ya taifa kufuzu kuingia kwenye kombe la dunia.

‘’ Siri  kubwa  ya mafanikio  ni mazoezi  Vijana hakuna kusema kiatu kimebana tunakwenda kuifunga Burundi ninachowaomba wana kagera wabunge wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na mikoa jirani twendeni Burundi tukaishangilie timu yetu’ alisema. 

Hata hivyo Amesema kuwa Rekodi ya Tanzania ni nzuri kwani timu ya watoto wa kike chini ya miaka 17 ilikaribishwa afrika kusini kimichezo na kuwabamiza  mabao 8-0 na kurudi Tanzania na kombe ikiwa  ni mara ya tatu kuchukua ubingwa.

No comments:

Post a Comment

Pages