HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 11, 2019

SERIKALI YA TANZANIA YAPOKEA FARU TISA

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiangalia mmoja  wa faru weusi  kati ya faru tisa ambao wapo kwenye banda maalum mara baada ya kushushwa kwenye ndege mara baada ya  kuwasili leo katika uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro wakiwa wametokea nchi ya Afrika Kusini. Faru hao wameletwa nchini ili  kuja kuongeza idadi ya faru waliopo kutokana vitendo vya ujangili kushamiri Sikh za nyuma . Wengine ni baadhi ya viongozi Taasisi za uhifadhi nchini pamoja na Wakuu wa mikoa ya Arusha na Kilimanjaro.

 

 

Na Mwandishi Wetu 

 

Serikali ya Tanzania imepokea faru weusi  tisa kutoka nchi ya Afrika ya Kusini ambao watapelekwa katika Hifadhi  mbalimbali nchini.


Faru hao wamepokelewa leo Septemba 10, 2019  na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiwa pamoja na viongozi mbalimbali katika uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro( KIA)

Akizungumza mara baada ya kupokea faru hao, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amesema tukio hilo ni la kihistoria kwa vile ni mara ya kwanza  kupokea idadi kubwa ya faru kwa wakati mmoja.

Hata hivyo, Mhe.Kanyasu amesema  idadi ya faru hao walikuwa kumi ambapo faru  mmoja kati ya hao  kumi alipoteza maisha wakati  akiwa njiani kuletwa nchini.

Mhe.Kanyasu amesema faru hao watalindwa kwa gharama yoyote ile ili kuhakikisha hawapungui kama ilivyotokea katika miaka 1970-1980.

Amesema tatizo la ujangili  ndiyo sababu kuu iliyopelekea kupungua kwa faru hali iliyopelekea maeneo mengine katika nchi faru hao kutoweka kabisa na sasa imebaki historia.

Aidha, Mhe.Kanyasu ametoa wito kwa jamii pamoja na Wahifadhi kuwa Wazalendo kwa kuwalinda faru hao ambapo kwa sasa Serikali inafanya jitihada ya kuzuia wasiweze kutoweka kabisa.

Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu amewashukuru Wadau wa Uhifadhi nchini hususan Uongozi wa Mfuko wa Grumet kwa jitihada kubwa za kuwezesha upatikanaji wa faru hao.

Amesema hadi hivi sasa  jitihada mbalimbali  ambazo zilichukuliwa na Serikali kwa kushirikiana na Wadau wa Uhifadhi nchini katika miaka ya 90  zimeanza kuzaa matunda katika Hifadhi nchini.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Grumeti amesema wayaendelea kushirikiana na Serikali mikakati yenye  maslahi kwa Taifa katika kuhifadhi wanyamspori

Ameeleza  kuwa ujio wa faru hao  ni hao ni utekelezaji  wa kuongez idadi ya faru katika makazi yao ya asili

Aidha, Mhe.Kanyasu amewataadhalisha watu wenye nia ovu wa kuhujumu faru hao hawatavumiliwa.

No comments:

Post a Comment

Pages