HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 13, 2019

Tigo yazindua ‘Office Internet’ kwa wafanyabiashara wadogo

Ofisa Mkuu wa Tigo Business, Pavan Ramdhani, akimkabidhi kifaa cha 'Routers' Mwandishi Mwandamizi wa Gazeti la TanzaniaDaima, Suleiman Msuya aliyeshinda bahati nasibu, baada ya uzinduzi wa huduma mpya ya ‘Office Internet’ (Picha na Mpiga Picha Wetu).


NA SULEIMAN MSUYA
KAMPUNI ya simu ya Tigo, kupitia kitengo chake cha Tigo Business imezinduzi huduma mpya ya ‘Office Internet’ ikiwalenga wafanyabiashara wadogo na wa kati nchini.
Afisa Mkuu wa Tigo Business, Pavan Ramdhani, aliwaambia waandishi na wateja wa Tigo kuwa, kuwa huduma hiyo ni ya kisasa na inaenda na wakati na imeshirikisha wataalamu wa Microsoft.
Ramdhani alisema huduma hiyo ina mfumo wa kisasa uliounganishwa na Microsoft hivyo kuifanya Tigo kuendelea kuwa kinara wa ubunifu na kuiwezesha kufanya biashara zake kwa malengo.
“Sambamba na uzinduzi wa  huduma ya ‘Home Internet’ uliyofanywa na Tigo hivi karibuni,  huduma ya ‘Office Internet’ inakuja na faida endelevu kwa wateja wenye biashara ndogo na za kati ambao hupendelea huduma za intaneti kwa mkataba. Hii inadhihirisha matumzi bora ya mtandao wa wenye kasi nchini Tanzania wa 4G+.
“Tulifanya kazi kwa ushirikiano wa karibu sana na wateja wetu, ambapo walituonyesha maeneo matatu muhimu yenye changamoto; Muda unaotumika kuunganisha huduma ya intaneti, Kasi ya huduma hiyo na ukosefu wa maana halisi,  Matumizi ya intaneti na zana zenye uhusiano na biashara,” alisema.
Kwa upande wake Kaimu Mkuu Mauzo Tigo, Niki Kazuka wana furaha kutangaza huduma hiyo ya aina yake hapa nchini na kuwaomba wafanyabiashara wadogo na kati kuitumia kibiashara.
“Office Internet ina huduma ya daraja la kwanza iliyounganishwa na mtandao wa Tigo 4G+,  wenye watumiaji wengi duniani kote chini ya ushirikiano wa Microsoft,” alisema.
Alisema huduma hiyo inatumika bila muunganisho wa waya, kwa maana ya kwamba mteja wao anatakiwa kuwasha kifaa chake cha Modem  au Router.
Mtaalam wa Biadhaa Kitengo cha Tigo Business, Brayan Swai alisema kifaa hicho kina uwezo wa kuunganisha vifaa 10 hadi 32 kwenye inteneti kwa mara moja.
“Microsoft 365 inaruhusu kufanya mambo mbalimbali ikiwamo utumaji wa barua pepe za kibiashara,  kutuma na kuhifadhi ujumbe katika mtandao, matumizi ya Microsoft katika masuala yote ya kibiashara ikiwamo mikutano ya moja kwa moja mtandaoni,” alisema.

No comments:

Post a Comment

Pages