HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 11, 2019

WAWEKEZAJI WACHANGAMKIA FURSA KAGERA

 Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti, akizungumza na wawekezaji katika seka ya ufugaji kutoka Rwanda ofisini kwake.



Na Lydia Lugakila, Bukoba

Wawekezaji kutoka nchi jirani sasa wapishana kuchangamkia uwekezaji kagera ni baada ya wiki ya uwekezaji kuwaonesha fursa.

Juhudi za viongozi wa Mkoa wa Kagera kuufanya mkoa huo kuwa kitovu cha uchumi wa nchi za Afrika Mashariki na Kati zilizoanzia katika Wiki ya Uwekezaji Kagera sasa zaanza kuzaa matunda ni baada ya kundi la wawekezaji kutoka nchi jirani ya Rwanda kuitikia wito wa kuwekeza mkoani humo.

Kundi hilo la Wawekezaji wapatao kumi ambao ni wamiliki wa makampuni mbalimbali ya biashara nchini Rwanda walioamua kuunda Kampuni moja ya uwekezaji mkoani Kagera katika Sekta ya ufugaji wa kisasa na kuanzisha kiwanda cha kusindika nyama wamewasili moani hapa Septemba 11 mwaka huu katika ofisini ya Mkuu wa Mkoa Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti ili kumweleza nia yao na kuwa wapo tayari kuwekeza katika ufugaji na kiwanda cha kusindika nyama.

 William Kawamala ni kiongozi wa wawekezaji hao kumi kutoka nchini Rwanda amemweleza Mkuu wa Mkoa Gaguti kuwa wapo tayari kuwekeza katika sekta ya ufugaji  wa kisasa wa ng’ombe katika Kampuni za  Ranchi za Taifa (NARCO) baada ya kupata fursa hiyo katika Wiki ya Uwekezaji Kagera iliyofanyika tarehe 12 hadi 17 Agosti, 2019.

“Sisi baada ya kushiriki Wiki ya Uwekezaji Kagera tulivutiwa kuwekeza katika Sekta ya ufugaji, na tuliporudi kwetu nchini Rwanda tulikaa pamoja na kukubaliana tujiunge kwa pamoja wafanyabiashara kumi ili kuanza uwekezaji mara moja, ndiyo maana tupo hapa ili kuanza hatua za awali pia tumekuja kuona maeneo ya kufugia na kuweka kiwanda..”  Amefafanua  Kawamala’’.

Mkuu wa Mkoa Gaguti amewakaribisha wawekezaji hao na kusema kuwa mkoa upo tayari kuwapa ushirikiano,  hatua ya kwanza amemwelekeza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NARCO Prof. Philemon Wambula pamoja na baadhi ya wataalam kutoka Sekretarieti ya mkoa  kuwaonesha maeneo yaliyotengwa ili wakubaliane nayo na taratibu  za kusajili kampuni na kuanza uwekezaji zianze mara moja.

“Baada ya Wiki ya Uwekezaji mwitikio umekuwa mkubwa sana wa wawekezaji kuja kwetu kuchangamkia fursa zilizopo Kagera na sisi tumejipanga tunawapokea na kuwaelekeza taratibu za uwekezaji, lakini jukumu letu ni kuhakikisha fursa zote ambazo wawekezaji wameziona wanazitumia katika uwekezaji ili kukuza uchumi wa mkoa wetu.” Alisisitiza Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Profesa Philemon Wambula Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni za Ranchi za Taifa (NARCO) alisema kuwa mkoa wa Kagera bado una fursa kubwa za uwekezaji katika sekta ya mifugo hasa katika viwanda vya kusindika nyama na maziwa pia uwekezaji katika malisho ya mifugo aidha, NARCO bado inayo maeneo makubwa ya kuwekeza. 

Wawekezaji hao kumi walieleza kuwa baada ya kuona maeneo wanataka kuwekeza katika ufugaji wa kisasa wa ng’ombe, ujenzi wa kiwanda cha kuchinja na kusindika nyama kwa viwango vya kimataifa. 

“Kwasasa baadhi ya Hoteli kubwa nchini Rwanda zimeanza kuagiza nyama kutoka nchi za Ulaya wakati tukifuga kisasa hapa Kagera tunaweza kuilisha Rwanda.”  walisisitiza Wawekezaji hao kutoka nchini Rwanda.

No comments:

Post a Comment

Pages