Na Tiganya Vincent
HALMASHAURI ya Wilaya ya Kaliua
imeomba kuidhinishiwa shilingi bilioni 38.7 ikiwa ni makisio ya mapato na matumizi ya mwaka ujao wa
fedha wa 2020/21.
Fedha hizo zinatokana na
makusanyo ya vyanzo mbalimbali ikiwemo ruzuku toka Serikali kuu na makusanyo ya
mapato ya ndani ya Halmashauri.
Kauli hiyo imetolewa leo na
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua Edwin Mashala wakati
wa kikao na Sekretaieti ya Mkoa wa Tabora cha kuchambua na kujadili mapendekezo ya
makisio ya mipango na
bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa kwa mwaka ujao wa fedha.
Alisema kati ya fedha hizo
bilioni 35 .4 ni ruzuku kutoka Serikali kuu na bilioni 3.2 zitatokana
na makusanyo yanayotokana na mapato ya ndani.
Mashala alisema
mapendekezo ya bejeti ijayo yamezingatia kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya
Wilaya , Vituo vya Afya Usinge, Mwongozo na Uyowa na kuendeleza ukamilishaji wa
miundombinu ya shule na huduma za elimu.
Alisema eneo jingine ni uimarishaji wa makusanyo ya ndani kwa
kutumia mfumo wa kielektroniki na kuongeza vyanzo vya mapato vipya ili kuongeza
mapato na uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia mikopo ya wanawake , vijana na
walemavu.
Mashala aliongeza kuwa kipaumbele kingine ni uchongaji wa
barabara katika maeneo yaliyopimwa na ulipaji wa fidia ya maeneo yalitwaliwa na
Halmashauri kwa shughuli za umma.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa
Tabora Hamis Mkunga aliwataka viongozi wa Halmashauri hiyo kuongeza juhudi
katika kuimarisha vyanzo vya makusanyo ili wawe na uwezo wa
kujitegemea ifikapo mwaka 2025 kama Serikali ilivyoagiza.
Kwa upande wa Katibu Tawala
Msaidizi Rukia Manduta alitaka Halmashauri kujitahidi kutozalisha madeni kwani
Serikali Kuu haitakuwa tayari kulipa madeni yao.
Alisema jambo la msingi ni kujitahidi kukusanya fedha kutokana
na mapato ya ndani ili waweze kulipa madeni yao.
Aidha Katibu Tawala Msaidizi huyo aliwakumbushia kuhakikisha wanatenga
wa fedha katika bajeti ijayo kwa ajili
ya ununuzi wa taulo za wanafunzi wa kike mashule, asilimia 10 kwa ajili ya mikopo
ya wanawake , vijana na walemavu na kutenga
fedha kwa ajili ya uendeshaji wa shule mpya
No comments:
Post a Comment