HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 27, 2020

DK. MWAKYEMBE KUTETA NA RIADHA

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe anatarajiwa kuwa na kikao  na uongozi wa Riadha pamoja na wadau wa mchezo huo kitakachofanyika Moshi mkoani Kilimanjaro, Jumapili Machi Mosi mwaka huu.

Kutokana na tukio hilo, Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), linapenda kuwaalika wadau wote wa mchezo wa Riadha wakiwamo makocha, waandaaji wa matukio mbalimbali ya mbio (Race Organiser), kuhudhuria kikao hicho.

Kikao hicho muhimu, kitafanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Ni mategemeo yetu RT, Wadau wengi wa mchezo wa Riadha watahudhuria bila kukosa kwa manufaa ya mchezo wetu, hasa ikizingatiwa siku hiyo ni siku ya mbio maarufu za Kilimanjaro Marathon.

IMETOLEWA NA:
Tullo Chambo
Msemaji RT
0752 46 21 03
27/02/2020

No comments:

Post a Comment

Pages