HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 21, 2020

TABORA WAIOMBA SERIKALI KUKICHUKUA KIWANDA CHA NYUZI

Na Tiganya Vincent

MKOA wa Tabora umeelezea kutoridhishwa na utendaji kazi wa Mmiliki wa Kiwanda cha Nyuzi Tabora (New Tabora Textile) na kutaka kichukuliwe na Serikali na kutafutwa  mwekezaji mwingine anayeweza kukiendesha kwa faida kwa ajili ya manufaa ya wakazi wa Mkoa huo na Taifa.

Kauli hiyo imetolewa jana na Katibu Tawala Msaidizi( Uchumi na Uwekezaji)  Mkoa wa Tabora Raphael Nyanda wakati  akiwasilisha taarifa ya uwekezaji kwa Mkoa wa Tabora kwa Wajumbe wa Kamati ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Tabora walipokuwa wakipokea taarifa ya utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Alisema kuwa Mwekezaji wa sasa ameshindwa kukifanya kiwanda hicho kwenda kisasa na kwa kulingana na soko la wakati huo na ujao na hivyo kutokuwa na faida kwa uchumi wa Mkoa na nchi.

Nyanda aliongeza kuwa Mwekezaji huyo anakwenda kinyume na lengo la Kiwanda hicho ambalo ilikuwa kununua pamba nyuzi kutoka vinu vya kuchambulia pamba na kuzalisha nyuzi kwa ajili ya kulisha viwanda vya nguo hapa nchini na nje ya nchi.

Alisema kuwa tayari Mkoa umeshaandika barua Ofisi ya waziri Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Wizara ya Viwanda na Msajiri ukipendekeza Kiwanda kiwe huru na kupewa mwekezaji mwingine.

Nyanya alisema Mwekezaji alipopewa Kiwanda hicho Viongozi mbalimbali wa ngazi ya wilaya hadi Taifa akiwemo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa alitembelea Kiwanda hicho mwaka 2018 na kuagiza kifufuliwe na kuanza kazi mara moja lakini Mwekezaji ameshindwa kutekeleza agizo hilo.

No comments:

Post a Comment

Pages