HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 04, 2020

MKURUGENZI MTENDAJI CRDB APEWA TUZO YA HESHIMA


Na Mwandishi Wetu

JARIDA mashuhuri duniani la African Leadership limempa tuzo ya heshima katika uongozi kwa mwaka 2019; Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela.

Utoaji wa tuzo hiyo ya nane kwa viongozi wa Afrika waliofanya mambo makubwa kwenye taasisi ama maeneo wanayoyaongoza ulifanyika hivi karibuni jijini Johannesburg, Afrika Kusini

Tuzo hiyo iliasisiwa ili kutambua mchango wa kiongozi katika Bara la Afrika ngazi ya wakurugenzi na namna anavyopenyeza biashara yake na kuwafikia wengine kwa urahisi na kuaminika katika kujenga imani na ushindani wa taasisi yake barani Afrika.

Akizungumzia tuzo hiyo ya heshima, ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo Machi 4,2020; Nsekela alisema anafurahi na kuipokea heshma hiyo huku akiwashukuru zaidi watanzania, wafanyakazi na wateja wa benki ya CRDB.

"Kwa unyenyekevu nimeipokea tuzo hii ya heshima nikitambua kwamba ni matokeo chanya ya juhudi, biashara na huduma zetu bora... ninawashukuru sana African Leadership Magazine kwa kutambua na kuithamini kazi yetu," alisema Nsekela.

Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Meja Jenerali mstaafu Gaudence Milanzi aliyeshuhudia utoaji wa tuzo hiyo ya heshima, alipongeza juhudi za Nsekela katika utendaji wake wa kuleta mabadiliko chanya kwenye Benki ya CRDB na sekta ya fedha Tanzania na Afrika.

Akipokea tuzo ya heshima kwa niaba ya Nsekela, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, TulliEsther Mwambapa alisema hiyo ni ishara ya uongozi imara wa benki yao na usimamizi madhubuti wa kanuni za msingi za uendeshaji wa taasisi hiyo kongwe ya fedha hapa nchini.

"Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Nsekela pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA) hiyo ni ishara kwamba utendaji wake kwenye sekta ya fedha ni bora ndio maana amepata tuzo hii... anafanya juhudi kubwa kuleta mabadiliko ya uendeshaji wa sekta hii ili iwe bora zaidi ndani na nje ya Tanzania.

"Nsekela anasaidia kuijenga vema sekta ya fedha kwa kusimamia miradi ya maendeleo kwa kukuza uchumi wa jamii," alisema Mwambapa.

Hafla ya utoaji wa Tuzo ya Heshima ilibebwa na kaulimbiu isemayo 'Afrika kwa Waafrika katika kuunganisha Bara lao' iliyohidhuriwa na wafanyabiashara na viongozi wasimamizi wa sera za fedha kutoka nchi mbalimbali Afrika akiwemo Naibu Rais wa Afrika Kusini, David Mabuza.

Viongozi wengine wa serikali waliokuwepo ni Deputy President, Republic of South Africaand Her Excellency, Nkosazana Dlamini-Zuma, Minister for Corporative Governance and Traditional Affairs, South Africa.

No comments:

Post a Comment

Pages