HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 04, 2020

RC TABORA ATAKA MAJINA YA WANAOJIUSISHA NA BIASHARA HARAMU YA MAZAO WATAJWE

NA TIGANYA VINCENT
 
MRAJISI Msaidizi wa Ushirika Mkoa  wa Tabora ameagiza kupeleka na kutaja majina ya watumishi na viongozi wanajihusisha na biashara haramu ya mazao ya biashara ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati wa Kikao cha Ushauri cha Mkoa(RCC)  wa Tabora cha kupitia mapendekezo ya bajeti ya 2020/21.

Alisema vitendo hivyo vinawadhofisha wakulima na kuwafanya kuendelea kuwa masikini na Halmashauri za Wilaya zinazolima mazao hao kupata mapato kidogo yanatoka na ushuru wa mazao.

Mwanri alisema haiwezekani kila wakati Ofisi ya Mrajisi Msaidizi inatoa taarifa kuwa kuna baadhi ya viongozi wa serikali, wa siasa na Vyama vya Ushirika  wamejiingiza kwenye biashara ya vishada na uuzaji wa pembejeo bila kuwataja majina.

Alisema kuwa Serikali kupitia Waziri Mkuu inashatoa maelekezo kuwa mtu akayeruhusiwa kuuza tumbaku ni yule ambaye ana shamba la tumbaku na zao hilo litauzwa kupitia ushirika.
Aidha Kamati hiyo ya ushauri ya Mkoa wa Tabora imeviomba Vyombo vya Usalama ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuchunguza kuwafuatilia wanajihusiha na vitendo hivyo ili wachukuliwe hatua za kisheria.
Ilisema vitendo hivyo ni kosa ikiwemo la rushwa na udanganyifu kwa ajili ya kumnyonya mkulima na kuibia Serikali mapato yake yanatokana na ushuru wa mazao.
Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu alisema kuna baadhi ya viongozi wanashiriki katika biashara chafu ya uuzaji na ukopeshaji wa wakulima fedha kwa riba kubwa na kuwafanya kuendelea kuwa masikini.
Alisema kuna baadhi ya wakulima wamekuwa wakikopesha pembejeo na fedha kwa mara mbili ya bei halali kwa madai kuwa pindi atakapovuna tumbaku ni lazima ampe sehemu ya tumbaku kama malipo ya deni.
Makungu alisema vitendo hivyo vimefanya wakulima wengi wakati wa kuuza tumbaku yao kubaki na fedha kidogo ikiwa sehemu kubwa inaenda katika deni.

No comments:

Post a Comment

Pages